Saturday, September 17, 2011

Mahaka ya kutete haki za binadamu yaombwa kuwashitaki viongozi wa Kanisa.

Mahakama ya kutete haki za binadamu yaombwa kuwashitaki viongozi wa Kanisa
. Chikago, Marekani - 17/09/2011. Kundi la kimataifa linaloshughulikia haki za wale wote aliotendewa maovu na kanisa Katoliki, limetaka kesi ifunguliwa zidi ya viongozi wa kanisa hilo. Kundi hilo limepeleka malalamiko yake kwenye mahakam ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu kwa msaada wa wanasheria wa kujitokea na kudai ya kuwa vitendo vilivyo fanywa watumishi wa kanisa Katoliki vinatakiwa kufuatiliwa kisheria na viongozi walio husika na kuficha siri lazima wafikishwe mahakamani kujibu mashitaka. Hata hivyo wanasheria wa kimataifa wana sema "itakuwa vigumu kwa mahakama hiyo kufuatilia kesi hiyo kutokana na baadhi ya vifungu vya sheria vilivyopo kuhusu uhalali wa kuendesha kesi hiyo." Papa Benedekt alisha zungumzia hali hiyo na kusema "nikitendo cha aibu kilicho fanywa na watumishi wa Kanisa la Katoliki na kuhaidi yakuwa atalishughulikia kwa undani zaidi."
Kanisa Katoliki limekuwa na wakati mgumu katika miaka ya hivi karibuni,baada ya kugundulika ya kuwa baadhi ya watumishi walikuwa wanashiriki katika vitendo vya kulawiti.
Serikali ya mpito ya Libya yakubaliwa Umoja wa mataifa. New York ,Marekani - 17/07/2011.Umoja wa mataifa umepitisha muswada wa kuikubali serikali ya mpito ya Libya kama mwakilishi wa nchi hiyo. Kukubalika huko kwa serikali ya mpito ya Libya kumekuja baada ya viongozi wa Ufaransa, Uingereza na Uturuki kufanya ziara za kiserikali nchini Libya kwa mara ya kwanza, tangu kuangushwa kwa serikali ya Muammar Gaddafi hivi karibuni. Mwakilishi wa Urusi katika umoja wa mataifa alisema " niwajibu wa jumuiya ya kimataifa kwa kushirikiana na umoja wa mataifa kuisaidia Libya ili kujenga miundo mbinu ya kisiasa ili kuweza kukuza demokrasia na kuleta amani nchini humo." Hata hivyo vikwazo vya anga bado vitaangaliwa kwa makini, japo kuwa Urusi inataka vikwazo hivyo viondolewe haraka iwekezekanavyo ili kurahisisha maendeleo ya ujenzi wa Libya. Wapalestina kudai utaifa wao New York. Lamalla, Marekani - 17.09.2011.Mamia ya Wapalestina wameandamana karibu miji yote iliyopo Palestina kuunga mkono uamuzi wa serikali kwenda Umoja wa Mataifa kudai haki ya Utaifa wa Wapalestina. Rais wa baraza la Wapalestina aliwa wahakikishia Wapalestina ya kuwa atafanya kila linalo takiwa ili kuliomba baraza la Umoja wa Mataifa kuunga mkono kwa Wapalestina kukubalika kuunda taifa huru la Kipalestina. Akikisisitiza hoja hiyo, rais Mohmoud Abbas alisema " kuna nchi zaidi ya 120 zimekubali kuunga mkono ombi letu, kufuatia hotuba ya rais Baraka Obama, aliyoitoa mwaka 2010 kwenye mkutano mkuu wa umoja wa mataifa ya kuwa mwaka 2011 tutakuwa wanachama kamili wa umoja wa mataifa." Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon alikubaliana na hoja ya Wapalestina kwa kusema " swala la Wapalestina linaeleweka na makubaliano ndiyo njia nzuri ya kuleta amani." Rais Mohmoud Abbas anatarajiwa kuwakilisha ombi lake hilo, baada ya hotuba ya tarehe 23. Septemba mwaka huu katika mkutano mkuu wa umoja wa mataifa.

No comments: