Tuesday, May 15, 2012

Francois Hollande aanza kazi yake urais rasmi leo nchi Ufaransa.

Francois Hollande aanza kazi yake urais rasmi leo nchi Ufaransa.

Paris, Ufaransa - 15/05/2012. Raia wa Ufaransa wapemepata rais mpya kutoka chama cha mrengo wa kushoto  cha Sosialisti tangu miaka 17 iliyo pita.
Francois Hollande ambaye alishinda uchaguzi wa rais hivi karibuni nchini Ufaransa aliapishwa rasmi leo kuwa rais wa Ufaransa baada ya Nicolas Sarkozy aliyekuwa rais kushindwa katika kura za kugombea kiti hicho cha urais wa Ufaransa kwa mara ya pili.
Rais Froncois Hollande alisema haya baada ya kuapishwa " ukurasa mpya umefunguliwa, ningependa kuwaapa huu ujumbe ya kuwa Wafaransa kuweni na imani, sisi ni taifa kubwa na huwa siku zote tuna pambana na kushinda magumu yanayo tukabili, na nahaidi ya kuwa  nitailinda na kuongoza kwa maadili bora ya ukweli, haki na usawa kwa kila Mfaransa."
Ushindi wa Francois Hollande umekuja baada ya kampeni yake kubwa ya kuhaidi kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi nchini Ufaransa kama akichaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo.


Luis Moreno Ocampo bado amsaka  Bosco Ntaganda na wenzake.

Hague, Uhollanzi - 15/05/2012. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za mauji na unyanyasaji wa haki za binadamu ipo mbioni kuhakikisha viongozi wa makundi ya kijeshi yaliyopo JD Kongo  wakamatwe.
Mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo Luis Moreno Ocampo alisema " kuna baru ya kutaka Bosco Ntaganda na Sylvestre Mudacumura wakamatwe ili waje wajibu mashitaka ya kuhusika na ubakaji, unyanyasaji na mauji, watu hawa ni hatari saana."
Maoni hayo ya Ocampo yamekuja baada ya habari kupatikana ya mkuwa jeshi la umoja wa mataifa lilipo nchini JD ya Kongo kushambuliwa na na wanachi kwa madai jeshi hilo linashindwa kuwalinda kutokana na mashambulizi yanayo fanywa na makundi ya kijeshi yanayo pingana na serikali ya JD Kongo.
Viongozi hao wakijeshi waliopo nchini JD Kongo wamekuwa wanashutumiwa kwa kuhusika katika uchafuzi wa amani kwa kusababisha mauaji na ubakaji ambao uamekuwa yakitokea kwa muda mrefu sasa.


Muuaji wa mwanasayansi wa Iran anyongwa.


Tehran, Iran - 15/05/2012. Raia wa Iran aliyekutwa na hatia ya kumuua raia mwenzake ambaye alikuwa mwanasayansi wa mambo ya kinyuklia amenyongwa.
Habari kutoka shirika la habari la Iran zilisema "Majid Jamali Fashi ambaye alikutwa na hatia ya kumuua mwanasayansi  Profesa Massoud Ali Mohamed kwa kumtegea bomu mwaka 2010 alinyongwa hivi karibuni.
"Mtuhumiwa huyo ambaye pia alikutwa na hatia ya kuwa jasusi aliyetumiwa na idara ya upelelezi wa Izrael (MOSSAD) na inaamikiwa alipewa kiasi cha dola za Kimarekani $ 120,000 baada ya kukamilisha mauaji hayo."
Hata hivyo Izreal haikutoa maelezo yoyote kuhusu kuhusu huusiano uliopo kati ya Majid Jamali Fashi na MOSSAD kwa kusema "Izrael huwa aijadili au kuongelea maswala ya usalama kinyume na sheria."
Mauaji ya wanasayansi wanao shughuliklia maswala ya kinyuklia yameistusha serikali ya Iran na kutupia lawama  Marekani na Izrael kuwa ndizo nchi zinazo panga mipango ya mauaji ya wanasayansi wake.
Hata hivyo Marekani na Izrael zimekanusha kuhusika na mipango hiyo kwa kudai ni uzushi ambao usiyo na msingi.


No comments: