Saturday, May 19, 2012

Baraka Obama atanga mabilioni ya dola kwa kilimo barani Afrika.

Chelsea ya twaa ubingwa wa kombe la Ulaya kwa mara ya kwanza.

Munich, Ujerumani - 19/05/2012. Chelsea imechukua ubingwa wa kombe vilabu bingwa vya Ulaya kwa mara ya kwanza baada ya kuishinda timu ya Bayern Munich kwa penati 4-3 baada ya dakika 120 kumalizika kwa kila timu kufunga goli 1- 1.
Bayern Munich ilikuwa ya kwanza kupata goli lake kwa kupitia Tomas Muller katika dakika ya 83 na Didier Drogba alisawazisha katika dakika 88, jambo ambalo lilifanya mchezo huo kuisha 1-1 kwenye dakika 90 na baadaye mchezo huo kuendelea kwa kuongezwa dakika 30 za ziada ambapo zilikwisha  1-1 na mchezo huo kuamuliwa kwa penati na Chelsea kuchukua ubingwa wa kombe la Ulaya kwa msimu wa 2012-13.

 Wakuu wa nchi za G-8 wakubaliana Uguriki kubaki ndani ya jumuiya ya Ulaya.

Camp Davis, Marekani - 19/05/2012. Viongozi wa nchi za G-8 wamekutana nchini Marekani  na wamekubaliana kwa pamoja Ugiriki inatakiwa kubakia ndani ya jumuiya ya Ulaya.
Viongozi hao kutoka Marekani, Ujerumani, Japan, Uingereza, Urusi, Ufaransa, Canada na Itali walisema kwa pamoja " tunakubaliana kwa pamoja Greek ibaki katika jumuiya ya Ulaya wakati hali ya kiuchumi ya nchi hiyo kuwekwa sawa."
Viongozi hao ambao wapo nchini Marekani wamezungumzia pia maswala ya Korea ya Kaskazini na Iran, nchi ambazo zinavutana nazo katika maswala ya kinyuklia.

Mabomu nchini Syria yakutwa na mashaka ya kidemokrasia.

Deir az Zor, Syria - 19/05/2012. Mlipuko mkubwa ulitokea baada ya gari moja iliyokuwa imepakiwa mabomu kulipuka  karibu na maenao ya ofisi za usalama wa kijeshi.
Mlipuko huo ambao ulisababisha vifo vya watu wapatao  tisa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa vibaya na kuharibu majengo pamoja na magari yaliyokuwa karibu.
Habari kutoka shirika la habari la serikali zilisema "mashambulizi hayo ni moja ya mbinu za wapinzani wa serikali wakisaidiwa na Al Qaeda."
Syria imekuwa ikikumbwa na milipuko ya mabomu tangu kuanza kwa mageuzi ya kidemokrasia amboyo yamekuwa yakileta misimamo tofauti kati ya serikali na wapinzani wake.

Rais Malawi kuingalia upya sheria ya kupinga ushoga.

 
Lilongwe, Malawi - 19/05/2012. Rais wa Malawi ametangaza yakuwa serikali yake itaiangalia upya sheria ya kupinga ushoga iliyopoyo pitishwa mwaka 1994.
Joyce Banda alisema baadhi ya sheria zilizopo  zinatakiwa kuangaliwa upya ikiwemo ile iliyo pitishwa kuhusu ushoga."
Pia rais Banda aliongezea kwa kusema " niwakati mgumu uliopo kwa serikali, kwani naogopa yakuwa kuwasili kwa rais wa Sudan Omar al Bashir  mwezi Julai kwenye mkutano wa nchi za Afrika kunaweza kuleta uhasama na nchi wahisani"
Rais Joyce Banda alichukua madaraka kufuatia kifo cha rais Mbingu wa Mutharika, na tangu kuingia madarakani nchi wahisani wameaanza kuendelea kutoa misaada, baada ya kuisimamisha kutokana na kupishana misimamo na nchi wahisani ikiwepo Uingereza.

Baraka Obama atanga mabilioni ya dola kwa kilimo barani Afrika. 

Washington, Marekani - 19/05/2012. Rais wa Marekani ametangaza yakuwa serikali ya Marekani itatoa kisa kikubwa cha pesa katika bara la Afrika ili kusaidia kilimo.
Baraka Obama " nijambo la kiiutu kusaidia bara la Afrika, a hakuna sababu kubwa inayo lifanya Afrika ishindwe kujilisha yenyewe.
"Serikali ya Marekani itatoa kiasi cha  dola za Kimalekani $3billion ambazo zitawezesha kuinua na kuimarisha kilimo bora na kuinua maisha ya wakazi wa Afrika."
Rais Baraka Obama, aliyatangaza hayo kabla ya kuanza kwa mkutano wa wakuu wa nchi G-8 ambao Obama atakuwa mwenyeji wa mkutano huo
Katika mkutano huo, viongozi wa nchi za Tanzania, Benin, Ghana na Ethiopia wamealikwa kushiriki katika mkutano huo.

Thabo Mbeki kujaribu kusuruhisha Wasudani.

Khartoun, Sudan - 19/05/2012.  Aliyekuwa rais wa Afrika ya Kusini amewasili nchini Sudan ili kujaribu kuleta usuruhishi wa kisiasa uliyopo kati ya Sudani Khartoum na Sudani ya Kusini.
Thabo Mbeki anatarajiwa kukutana na rais wa Sudan Omar al Bashir, wakati mapigano kati ya jeshi la Khartoum na Juba.
Sudan ya Kusini na Sudan - Khartoum zimekuwa zikivutana katika swala la mpaka ambao unazikutatisha nchi hizo mbili, ambapo inaaminika kwenye eneo hilo kuna malighafi za asili ambazo ni kiini cha uchumi wa kila upande wa nchi.

No comments: