Monday, May 21, 2012

Ikulu ya Mali yavamiwa na rais ajeruhiwa vibaya na waandamanaji.

Waafghanistan kukabidhiwa ulinzi na usalama wa nchi yao na NATO 2014.

Chikago, Marekani - 21/05/2012.Viongozi wa nchi wanajumuiya wa nchi za  North Atlantic Treaty Organisation NATO, wamekubaliana kwa pamoja ya kuondoa majeshi ya NATO kuanzia 2013 nchi Afghanistan.
Viongozi hao ambao walikutana nchi Marekani Chikago, na kukubaliana ya kuwa uondokaji wa wanajeshi wa NATO utaanza taratibu naifikapo 2014 majeshi yote yatakuwa yamesha ondoka nchi Afghanistan.
Rais Baraka Obama ambaye alikuwa mwenyeji wa mkutano huo, alisema " nchi za jumuiya ya NATO 27  kuanzia mwaka 2014 swala la usalama wa Afghanistan litakuwa mikoni mwa jeshi Afghanistan, tutatoa misaada ya kimavunzo ili jeshi hilo liweze kuimarika vyema katika kulinda nchi ya Afghanistan."
Uamuzi huo wa viongozi wa wakuu wa NATO utafikisha kileleni vita vilivyo chukua miaka kumu katika kupambana chimbuko la ugaidi lililo kuwa na mizizi nchini Afghanistan. 

Ikulu ya Mali yavamiwa na rais ajeruhiwa vibaya na waandamanaji.

Bamako, Mali - 21/05/2012. Waandamanaji wamevamia Ikulu  ya rais wa  Mali na kumjeruhi vibaya rais wa mpito wa nchi hiyo.
Dioncounda Traore ambaye alikutwa na waandamanaji hao wakati akiwa ofisini na kupigwa hadi kupoteza fahamu na huku waandamanaji wakisema "hatukutaki kuwa rais na hatutaki matwakwa ya ECOWAS."
Msemaji wa hospitali aliyo lazwa rais huyo wa mali  Sekou Yuttara alisema "Dioncounda Traore aliletwa hapa hospitali akiwa hajitambuhi na ameumia vibaya." 
Diocounda Traore alichaguliwa kuongoza nchi katika kipindi cha mpito ili kuunda serikali baada ya makubaliano ya jeshi la Mali ambalo  jeshi lilifanya  mapinduzi ya kumng'oa madarakani rais  Amadou Toumani Toure wezi Machi 2012.

Mazishi ya aliyetumiwa kuangusha ndege ya Pan Am 103 yafanyika leo Trpol.

Tripol, Libya - 21/05/2012. Aliye kuwa mtuhumiwa na kukutwa na hatia  na mahakama ya kuingusha ndege ya Pan AM 103 amefanywa mazishi yake leo baada ya kufariki dunia jana.
Abdel Basset al Megrahi 60, alifariki duni kutokana na ugonjwa wa kansa ambao ulikuwa ukimsumbua kwa muda mrefu tangu akiwa gerezani nchini Scotland.
Abdle Nassar kaka wa marehemu Abdel Basset Megrahi alisema " hali ya ndugu yangu ilianza kuwa mbaya baaday ya kufanyika mapinduzi ya kuing'oa serikali ya Muammar Gaddafi, kwani dawa alizo kuwa nazo ziilibiwa baada ya kuvamiwa na hadi kifo cha Megrahi hakukuwa na mganga wa kumwangalia."
Watu wapatao 100 waliudhuria katika mazishi, na hapakuwepo na viongozi wa serikali ya mpito. 
Abdel Besset Megrahi alizaliwa mwaka 1952 na alisoma Marekani na kuishi Uingereza mapema miaka ya 1970.

Wakuu wa serikali ya Iran wakutana na Mkuu wa usimamizi wa maswala ya Kinyuklia duniani.

Tehran, Iran - 21/05/2012. Mkuu wa shirika linalo simamia maswala ya kiatomiki na nyuklia duniani International Atomic Energy Agency IAEA amewasili nchini Iran.
Yukiya Amano aliwasili nchini Iran na kufanya mazungumzo na mkuu wa maswala ya kinyuklia ya Iran Fereydoun Abbas Daveni.
Baada ya  mkutano huo Fereydoun Abbas Daveni alisema "tumefanya mazungumzo yenye uwazi ambao hauna kutiliana mashaka na kufanikisha maendeleo."
Yukiya Amano pia alikutana Saeed Jalili  msemaji mkuu wa maswala ya kinyukia ya Iran na waziri wa mambo ya nje  Ali Akbar Salehi.
Mkuu huyo wa shirika la kusimamia maswala ya kinyuklia ya kimataifa ametembelea Iran kabla ya mkutano utakao fanyika baghdad Irak kati ya Iran na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa ili kujadili mpango mzima wa nyuklia ya Iran.

No comments: