Ufaransa yapata rais mpya Francois Hollande na Nikolas Sarkozy ashindwa uchaguzi.
Paris, Ufaransa - 06/04/2012. Matokeo ya uchaguzi nchini Ufaransa yamemng'oa madarakani rais wa sasa wa nchi hiyo Nikolas Sarkozy.
Katika matokea ya uchaguzi huo aliyekuwa mpinzani wa rais Sarkozy, Hollande ambaye anatarajiwa kuchukua ofisi ya urais pindipo atakapo apishwa alishinda kwa kupata asilimia 52% zidi ya Sarkozy 48%
Nikolas Sarkozy alisema " nimekubali kushindwa na watu wa Ufaransa wameongea kupitia kura zao."
Naye Francois Hollande ambaye ameshinda uchaguzi huo alisema " wananchi nawashurkuru kwa kunipa nafasi ya kuwa rais wa Ufaransa, na nitaifanya kwa moyo mmoja na kuilinda Ufaransa na watu wote Waufaransa kuwa sawa na kupata haki sawa kuanzai mtoto hadi mkubwa.
"Ufaransa ni ya watu wote, kwani tumekuwa tukigawanywa na kuanzaia sasa ni mwisho na hakuna mtu ataruhusiwa kufanya hivyo na niwajibu wangu kutimiza ya kuwa kila Mfaransa lazima ashirki katika kujenga taifa letu na lazima tuaandae taifa la vijana wa kesho wa Kifaransa na sisi ni Wafaransa na lazima tujue hili.
"Amani, usawa na haki za binadamu na kila ambacho kinahitajika kwa binadamu lazima kila Mfaransa apate viva Ufaransa."
Matokeo ya uchaguzi nchini Ufaransa nchini Ufaransa yalikuwa yanatazamiwa tangu hapo mwanzo yalikuwa
ya vuta ni kute kati ya Sarkozy na Hollende kutokana na kupishana kimirengo ya kisiasa.
Mamia waandamana kupinga kuapishwa kwa Vladmir Putin.
Kufuatia maaandamano hayo watu wapatao 400 wamekamatwa na polisi kwa kufanya vurugu kinyume na sheria.
Habari kutoka kwa msemaji wa polisi zinasema " watu 20,000 wameudhuria katika maandamano hayo.
Waandamanaji hao walikuwa wamebeba mabango yaliyo andikwa " tumechokwa kudanganywa."
Tangu kuchaguliwa kwa Vladimir Putin kuwa rais, Urusi imekuwa ikikumbwa na maandamano ya hapa na pale kwa kupinga kitecho hicho cha kuchaguliwa kwake kuwa rais.
Baraka Obama aanza kampeni za uchaguzi rasmi.
Columbus, Marekani - 06/05/2012. Rais wa Marekani ameanza kampeni ya urais nchini humo ambao unatazamiwa kufanyika mwaka huu.
Baraka Obama alisema " Demokrati watashinda uchaguzi kwa kutumia mikakati yake ile ile ya kuwahusisha wananchi kwa kuwatembelea mlango kwa mlango mtaa kwa mtaa ili kuwahakikishia Wamarekani ya kuwa bado wanauwezo wa kungoza nchi.
" Lazima tukumbuke ya kuwa tunasonga mbele na haturudi nyuma."
Rais Baraka Obama anatarajiwa na kugombania urais na mpinzania wake wa chama cha Republikani Mitt Romney ambaye amehaidi pia kuwa atamshinda Baraka Obama.
Wasudani wakubaliana na mpango wa Umoja wa Afrika.
Adis Ababa, Ethiopia - 06/05/2012. Mpango wa kuleta amani nchini Sudan ambao ulipendekezwa na umoja wa nchi za Africa ili kuleta amani ubekubalika.
Sudan na Sudai ya Kusini zimekubaliana kutimiza mpango wa kuleta amani kawati ya nchi hizo mbili ambao ulipendekezwa ili kuhakikisha yakuwa amani inakuwepo.
Mpango huo wa kuwepo wa kuwa mbinu saba ambao utazikutanisha nchi hizo mbili katika meza ili kujadili ni kwa jinsi gani amani itakuwepo kati yao.
No comments:
Post a Comment