Monday, May 14, 2012

Rais Hugo Chavez amaliza matibabu yake nchini Kuba

Rais Hugo Chavez amaliza matibabu yake nchini Kuba.

Karakas, Venezuela - 14/05/2012. Rais wa Venezuela ametangaza ya kuwa matibabu saratani (kansa)  aliyokuwa akifanyiwa nchini Kuba yamemalizika salama.
Rais Hugo Chavez 57 alisema" siku chache zilizo pita nilimaliza mzunguko wa matibabu yangu.
Nimekuja na matumaini makubwa yakuwa afya yangu itazidi kuwa nzuri na haya yote ni Mungu ana nitazidi kumwomba Mungu, siku zote tumwombe  Mungu atupe afya na uzima ili tuweze kumtumikia na kufanya kazi aliyo tuagiaza."
"Kwa baraka za Mungu na umwili wa askari ambao umeshughurikiwa na waganga kikamilifu, nitarudi  vitani mstari wa mbele katika kuendeleza mapinduzi ya kumomboa kila mwana Venezuela.
Nawashukuru wananchi wa wote wa Venezuela kwa maombi yenu na bila kuwasahahu wanachi wa Kuba chini ya Uongozi wa Raul Kastro na kaka yeke Fidel Kastro kwa kunipatia matibabu."
Hugo Chavez ambaye ametawala tangu 1999 amakuwa akienda nchi Kuba ili kufanyiwa matibabu ya kansa ambayo iligunduliwa na waganga wakati wa kuchunguza mwenendo wa afya yake.

Mmoja wa msaidizi wa Joseph Kony akamatwa.

Kampala, Uganda - 14/05/2012. Serikali ya Uganda imethibitisha kukamatwa kwa aliyekuwa mmoja ya viongoziwa kundi la Lord's Resistance Army (LRA) linalopingana na serikali ya Uganda.
Ceaser Achellam alikamatwa  nchi ya Afrika ya Kati kufuatia mipango ya kijeshi inayo endelea ya kutaka kuwakamata viongozi na wapiganaji wa LRA.
Msemaji wa jeshi la Uganda Felix Kulaigye alisema " kukamatwa kwa Achellema ni mafanikio makubwa kwani kutapunguza makali ya LRA, huyu Achelle ni mmoja wa samaki wakubwa wa LRA."
Serikali ya Uganda kwa msaada wa serikali ya Marekani zimekuwa zikimsaka kiongozi wa RLA Joseph Kony ambaye anadaiwa kuvuruga amani ya Waganda kwa muda wa miaka mingi sasa.

Umoja wa Mataifa wapitisha muswada wa kulinda ardhi za wenyeji.

New York, Marekani - 14/05/2012. Umoja wa Mataifa umekubali muswaada wa kihiyari  wa kusimamisha unyakuliwaji wa ardhi.
Muswaada huo ambao unazitaka serikali zote duniani, hasa zile zinazo tawala nchi masikini kusimamia haki za wanchi wao kikamilifu na kutouza au kukodisha ardhi hizo kwa makampuni ya kimataifa kwa kisingizio yanaleta maendeleo.
Maelezo yaliyo tolewa na  shirika la kimataifa la OXFARM yanaripoti ya kuwa kiasi cha heka million 200 zenye ukubwa wa Uingereza zimenunuliwa au kukodishwa na makampuni ya kimataifa katika nchi za Afrika na Asia."
Clara Jamart msemaji wa OXFARM alisema " kupitishwa kwa mswada huo ni mwanzo, kwani imechukua zaidi ya miaka mitatu ili kufanikisha muswada huu."
Kupitishwa kwa muswada huo kumekuja baada ya wasiwasi kuku ya kuwa makampuni ya kimataifa ya kutoka nchi tajiri yamekuwa yakitumia uwezo walionao kupata ardhi na hata kuwafanya wenye nchi kuwa na wakati mgumu kimakao hasa katika nchi za Ethiopia, Sudani ya Kusini, DR Kongo. 

NATO yaombwa kufanya uchunguzi vita vya Libya.

Gevena, Uswisi -14/o5/2012. Shirika linalo shughulikia na kusimamia haki za binadamu limetoa maelezo ya kuwa vita vilivyo ongozwa NATO ili kumng'oa Muammar Gaddafi vilisababisha mauji ya watu wasiyo na hatia.
Idara inayo simamia haki hizo ilisema " zaid ya watu 72 waliuwawa bila makosa kutokana na mashambulizi ya mabomu  ya anga yaliyofanywa na jeshi la NATO.
"Na NATO inabidi kufikilia swala kiuwajibikaji hilo kiundani zaidi."
Hata hivyo msemaji wa NATO Oana  Lungescu alisema " mashambulizi yote yaliyofanywa na NATO nchini Libya yalifuata sheria za kijeshi na yalifanywa katika maeneo yaliyo kuwa ya kijeshi, lakini katika hali ya kivita maisha ya watu huwa yanapotea kutokana na hali halisi.
"NATO ilifanya kila njia kuepuka kuleta maafa kwa raia na mali zao na kutoweka maisha yao hatarini."
Vita nchini Libya vilioongozwa na NATO kuwasaidia waliokuwa wanapinga serikali ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Muammar Gaddafi ambaye uwawa katika mapinduzi hayo.

No comments: