Sunday, May 20, 2012

Mshutumiwa wa mlipuko wa ndege ya Pan Am 103 afariki dunia.

Mshutumiwa wa mlipuko wa ndege ya Pan Am 103 afariki dunia.


Tripol, Libya - 20/05/2012. Raia wa  Libya ambaye alidai ya kuwa hakuwa na makosa ya kuhusika na mlipuko wa ndege ya shirika la Pan Am 103 mwaka 1988 amefariki dunia.
Abdelbeset Ali Mohmed al Megrahi 60, ye alikutwa na hatia na kuhukumiwa kwenda jela  miaka 27 kwa kosa la kuhusika katika ulipuaji wa ndege iliyo kuwa imebeba watu 270 ambapo watu wote walio kuwepo kwenye ndege hiyo walifariki dunia.
Abdulhakimu  ndugu wa  marehemu alisema " Abdelset A.M. Megrahi alifariki saa saba mchana 13:00 kwa saa za Libya."
Abdelbeset Ali Mohamed al Megrahi alihukumiwa kwenda jela mwaka 2001 nchini Scotland na baadaye aliachiwa huru   mwaka 2009 baada ya wauguzi kugundua ya kuwa alikuwa na ugonjwa wa kansa na kuruhusiwa kurudi nchini mwake Libya ambapo ilisadikiwa angeishi miezi mitatu, lakini aliweza kuishi miaka mitatu zaidi.

Vatikani yakumbwa na mtetemo wa uvumi wa habari.

Vatikan, Vatikn City - 20/05/2012. Papa Benedikt XVI ameteua  kamati maalumu ili kuchunguza kashfa za rushwa na matumizi  mabaya ya mzunguko wa pesa ambazo zimeenea hivi karibuni.
Kamati hiyo ambayo itashughulikia kiundani na kupata majibu ilikujua kama upo ukweli wa habari hizo.
Msemaji  wa Vatican Padri Federico Lombard alisema " kusambazwa ka habari hizo kumevunja sheria ya  na hipo haja kufuatilia ili sheria zichukuliwe."
Habari hizo pia  zina aminika kuelezea maisha ya binafsi ya Papa Benedikt VXI.

Mamia wapambana na polisi nchi Marekani.

Chicago, Marekani - 20/05/2012. Mamia ya watu waandamanaji katika jiji la Chicago wamepambana na polisi ambao walikuwa wanawazuia wasielekee kwenye eneo ambalo wakuu wa NATO wanafanya mkutana ili kujadili hali halisi ya shirikisho hilo.
 Kwa mujibu wa habari kutoka kwenye mkutano huo zinasema " moja ya swala muhimu ambalo litajadiliwa ni Afghanistan, "ambapo badhi ya nchi wanachama wa NATO wamesha tangaza kutoa majeshi yao nchini humo.
Katibu mkuu wa NATO Anders Fogh Rasmussen alisema " namatumaini ya kuwa swala la kuisaidia Afghanistan katika kulinda usalama wake litatiliwa mkazo na nchi za NATO, jambo ambalo litakuwa na faida kwa NATO na Waafghanistan."
Kwenye mkutano huo, rais wa Ufaransa Franois Hollande' atakuwa anaudhuria mkutano huo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais wa Ufaransa siku chache zilizo pita.

Chama cha Repabrikan cha Marekani chapitisha nguvu za kivita kwa Iran.

Washington, Marekani - 20/05/2012. Bunge la chama cha Republikan nchini Marekani limepiga kura na kupitisha muswaada wa kuishambulia Iran kama ikionekana usalama wa kinyuklia kwa Marekani.
Kura hizo zilizo pigwa 229 - 120 ambazo ziliunga mkono mswaadahuo.
Kwa mujibu wa katiba ya Mareakani katika maswala ya kiulinzi inasema " sheria  ya uamuzi wa ulinzi na usalama wa taifa itatumika kama ikihitajika katika kulinda usalama ikiwemo matumizi ya nguvu ya kijeshi."
Uamuzi wa bunge hilo umekuja wakati Marakani na Iran wanavutana katika mswala ya Iran kuwa na nyuklia.

Umoja wa Matifa waiwekea vikwazo Guinea Bissau.

New York, Marekani - 20/05/2012. Kamati ya usalama ya Umoja wa Matifa imeiwekea  vikwazo  serikali ya kijeshi Guinea Bissau baada ya kuchelewa kurudisha madaraka katika serikali ya kiraia.
Vikwazo hivyo ambavyo vimewekwa kwa viongozi wa kijeshi kutoweza kusafiri na kuhusishwa katika maswala ya kimataifa kama serikali.
Kamati hii iliamua kwa pamoja kwa kuiwekea Guinea Bissau  vikwazo vya kutoweza kununua siraha na matumizi ya aina yoyote ya kipesa.
Uamuzi huo umekuja kufuatia mapinduzi ya ambayo yamekuwa yakiikumba Guinea Bissau tangu mwaka 1974 tangu kupata uhuru kutoka kwa Wareno.

No comments: