Thursday, May 24, 2012

Ugiriki yatakiwa kukamilisha matakwa ya nchi za Umoja wa Ulaya.

Rais wa zamani wa Tunisia huenda akahukumiwa adhabu ya kifo.



Tunisia, Tunis - 24/05/2012. Mwanasheria wa kijeshi ameiomba mahakama kumpa adhabu ya kifo aliyekuwa rais wa Tunisia aliyepinduliwa kutokana na maanamano ya wananchi mwaka 2011.
Mwanasheria huyo aliiomba mahakama kutoa adhabu kali ya kifo kwa  Ben Ali kwa  kusababisha mauaji ya watu 300 katika mji wa Kasserine, Tala, Kairouan na Tajrouine.
Zine al Abidine Beni Ali ambaye alikimbilia nchi Saud Arabia, January/14/2011 na kuachia madaraka, amesha hukumiwa kwenda jela, wakati hayupo nchini Tunisia kwa makoso ya kula rushwa na kutumia mali ya umma vibaya.
Ben Ali ambaye alitawala Tunisia kwa muda wa miaka 23 anashutumiwa kwa kuongoza nchi vibaya, kula rushwa na kuonea wanchi kwa kutumia  vyombo vya dola.

Ugiriki yatakiwa kukamilisha matakwa ya nchi za Umoja wa Ulaya.


Brussels, Ubeligiji - 24/05/2012. Viongozi wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya wamemaliza mkutano wao na kusisitiza ya kuwa Ugiriki lazima ikamilishe matakwa mkataba wa mabadiriko ya kiuchumi.
Rasi wa jumuiya ya Ulaya Herman Van Rompuy alisema " tunataka Ugiriki kubakia kuwa nchi mwanachama wa jumuiya ya Ulaya.
"Natunategemea ya kuwa baada ya uchaguzi nchi Ugiriki, serikali itakayo chaguliwa itafanya uamuzi bora ili iweze kusaidiwa kuinua uchumi wa nchi hiyo."
Mkutano huo wa viongozi wa nchi wanachama wa nchi za jumuiya ya Ulaya wamekutana ili kujadili hai halisi ya kiuchumi za nchi wanachama ili kuweka mkakati wa kujikwamua na myumbo wa uchumi uliopo kwa sasa.

Iran yatishia kujitoa katika mazungumzo na nchi za 5+1.

Baghdad, Irak - 24/05/2012. Serikali ya Iran imetishia kujitoa katika mazungumzo yanayo endelea kati yake na nchi za Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, China na Urusi yanayo fanyika nchi Irak- Baghdad.
Kwa mujibu wa habari zinasema " nchi hizo tano ambazo ni wanchama wa kamati ya usalama ya umoja wa mataifa zimeshindwa kufikiana na matakwa ya Iran, kwani Iran inadai yakuwa mswada ulio pendekezwa hauna mabadiliko."
Hata hivyo Catherine Ashton waziri wa mambo ya kigeni wa jumuiya ya Ulaya aliongea na mwakilishi wa Iran katika majadiliano ya kinyuklia Saeed Jalili na Catherine Ashton alipo ulizwa nini kiliongelewa katika mkutano huo hakutoa jibu.
Mvutano kati ya Iran na  mradi wake wa kinyuklia na nchi za Ulaya Magharibi umepelekea Iran kuwekewa vikwazo na huku Iran ikidai yakuwa in haki ya kuendelea na mradi wake wa kinyuklia.

anchi wa Izrael wataka wakimbizi wa Kiafrika warudishwe kwao.

Tel-Aviv, Izrael - 24/05/2012. Maelfu ya wananchi nchi Izrael wamenadamana  kupinga kiterndo cha kuongezeka wakimbizi wa Kiafrika nchi humo.
Maandamano hayo ambayo yaliongozwa na  Michael Ben Ari ambaye ni mbuge kupitaia chama cha National  Union Part na Ben-Guir na Baruch Marzel ambao ni waandishi wa habari wenye msimamo mkali wa kisiasa wa upande wa kulia.
Waandamani hao walishika mabango yakupinga na kuilaumu serikali ya Benyamin Tetanyahu kwa kudai ya kuwa haifanyi lolote katika kuwaondoa wakimbizi nchini humo.
Izrael imekuwa na wakimbizi kutoka Sudan ya Kusini ambao wengi wao wameishi kwa muda mrefu nchini Izrael.

Ndege aina ya drone kutumika katika kuzuia ghasia.

Texas, Marekani - 24/05/2012. Polisi nchini Marekani wataweza kutumia ndege aina ya drone katika kutuliza ghasia.
Randy McDaniel ambaye ni mmoja wa  maafiasa wa polisi Texas alisema " hii itasaidia kuimarisha usalama hasa wakati wa vurugu."
Catherine Crump ambaye ni mfanayakazi wa American Civil Liberties Union alisema 2 halitakuwa jambo la busara ikiwa  ndege hizo zitaanza kutumika, kwani zinaweze leta madhara makubwa tofauti na polisi wa kawaida ambao huwa wapo katika matukio."
Ndege hizo aina ya drone zitakuwa na uwezo wa kubebe mabomu ya machozi na risasi zenye raba ambazo maranyingi utumika katika kuzuia ghasia.

No comments: