Wednesday, May 16, 2012

Charles Taylor adai mashahidi zidi yake walilipwa pesa

Charles Taylor adai walio toa ushahidi zidi yake walilipwa pesa.

Hague, Uhollanzi - 16/05/2012. Aliye kuwa rais wa Liberia na ambaye amekutwa na hatia ya kukiuka haki za binadamu na koti ya kutetea haki za binadamu amelaumu ya kuwa mashahidi walio kuja kutoa ushahidi zidi yake walipwa pesa.
Charles Taylor  64, alisema " Napenda kusema ya kuwa mashahidi walio kuja kutoa ushahidi zidi yangu walipewa pesa/kununuliwa na hata kutishiwa kushitakiwa ikiwa watakataa kuja kutoa ushahidi.
"Sikuwa na hatarisha maisha ya jamii kama inavyo daiwa, bali nilichokuwa najua ya kuwa ikiwa hakuna amani Sierra Leone, basi hata Liberia hakuta kuwa na amani.
"Mimi napinga na kulaani vitendo vyote vya kinyama, na ningependa uamuzi utakao tolewa na majiji uwe wa haki kuzingatia kiapo cha kazi zenu kwani mimi sasa ni mtu mzima na watoto naitwa babu. Vilevile ningependa kutoa masikitiko yangu kwa wale wote walio pata shida wakati wa vita. alisema Charles Taylor
"Japokuwa nipo hapa  inashangaza ya kuwa  viongozi wa nchi za Magharibi ambao wanauzia siraha makundi yanayo pigana kila sehemu na hasa bara la Afrika hakuna hata mmoja wao ambaye amesha wahi kushitakiwa au kushutumiwa kuhusika na vita na huu ndo ukweli wenyewe."
Wakili wa mahakama hiyo aliomba mahakama impe kifungo cha miaka 80 bwana Charlea Taylor
 wakati wa  kuhumu yake  mnomo tarehe 30 mwezi Mei 2012, atatumika kifungo chake nchi Uingereza kutokana  na makubaliano ya awali.
Hata hivyo mwana sheria anaye mwakilisha Charles Taylor alisema upo uwezekano wa kukata rufaa zidi ya adhabu ya kifungo itakapo tolewa.

Jeshi la Umoja wa Ulaya  la fanya mashambulizi nchi Somalia.

Haradhere, Somalia - 16/05/2012. Jeshi la nchi za jumuiya ya Ulaya limefanya mashambulizi kwa ndani ya Somalia kwa mara kwanza tangu kuanza ulinzi katika eneo hilo.
Jeshi hilo ambalo lilisafirishwa na helikopta hadi bandari Haradhere, ambayo inaamini kuwa kitovu cha maharamia ambao huvamia meli zinazo pita katika maeneo ya bahari  karibu na Somalia.
Bile Hussein ambaye ni msemajiwa wa  moja ya makundi ambayo yanashughurika na uharamia alisema " boti zao zenye mwendo wa kasi zilishambuliwa, pia baadhi ya maeneo yatu na vifaa vimeharibiwa vibaya na jeshi hilo la umoja wa Ulaya."
Serikali mpito ya Somalia   nayo ilithibitisha mashambyulizi hayo kwa kusema "mashambulizi hayo yalitokea kwa ushirikiano wa pamoja kati ya jeshi la Somalia na jeshi la umoja wa Ulaya."
maharamia waliopo nchi Somalia wamekuwa wakiziteka nyara meli zinazo pita katika maeneo yaliyopo karibu na bahari ya Somalia, nakusababisha hali ya uslama kuwa mashakani, jambo ambalo lili ifanya jumuiya ya kimataifa kuamua kuweka ulinzi katika maeneo hayo.

Serikali ya China ya chukuzwa na Serikali ya Uingereza.

Beijing, China - 16/05/2012.  Serikali ya China imelaani kitendo cha waziri mkuu wa Uingereza kukutana kiongozi wa kidini wa  Watibeti Dalai Lama.
Habari kutoka ofisi ya mambo ya nje ya China zilisema " kitendo hicho si cha busara na kinaingilia mambo ya ndani ya China na hakitaleta maantiki."
Nazo habari kutoka ofisi ya waziri mkuu wa Uingereza zinasema " waziri mkuu kukutana na Dalai Lama lilikuwa jambo muhimu, lakini wasingependa  swala hilo lilete kutoelewana kati ya China na Uingereza."
Dalai Lama ambaye alikimbia kutoka Tibeti 1959 na kufanya makazi yake Dharamsla India, baada ya jaribio la kutaka kuingausha serikali ya China kushindwa

Mji wa Mombasa wastushwa kwa mlipuko wa bomu.

Mombasa, Kenya - 16/05/2012. Wakazi wa mji wa  Mombasa nchini Kenya walistuliwa na mlipuko wa bomu uliotokea katika bar moja na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine watano kujeruhiwa vibaya.
Mashambulizi hayo ya bomu yalitokea katika bar ya Bella Vista Club, baada ya watu wenye sirjha kuzuiliwa kuingia ndani na ndipo walipo rusha bomu ndani ya  bar hiyo.
Mkuu wa Polisi Mombasa Aggrey Adoli alismema " watu waliofanya mashambulizi, kwanza walianza kufyatua risasi na kumjeruhi mmoja wa walinzi na baadaye kurusha bomu."
Kenya imekuwa ikishambuliwa na mabomu kwa muda sasa  tangu jeshi la nchi hiyo kuingia nchini Somalia ili kupambana na kundi la Al Shabab ambalo linasadikiwa kushirikiana na kundi la Al Qaeda.

No comments: