Wednesday, May 23, 2012

Muuguzi aliye husika katika kifo cha Osama bin Laden afungwa jela miaka 33.

Urusi yazidi kujimarisha kiulinzi.


Moscow, Urusi - 23/-5/2012. Urusi imefanikiwa kurusha siraha ( bomu) linalo julikana kama intercontinental ballistic missile ambayo inauwezo wa kupambana na kubomoa siraha ya ina yoyote.
Habari kutoka wizara ya ulinzi ya Urusi zilisema " majaribio hayo yalifanyika kwenye eneo la Plesetsk."
Jaribio hilo la Urusi limekuja wakati Marekani inajadili mpango wa kuweka mitambo yake ya kiulinzi katika bara la Ulaya, jambo ambalo Urusi bado haijahafikiana na Marekani katika swala hilo.
Hata hivyo Marekani imekuwa ikisisitiza ya kuwa mitambo hiyo ya kiulinzi ni kwa ajili ya kuzilinda nchi wanacham wa NATO.

eshi la JM ya Kongo lapata wakati mgumu wa kulinda nchi.
Kinshasa, Jamuhuri ya Kidemokrasi Kongo - 23/05/2012. Jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, limelaumiwa kwa kutotimiza kiapo cha kulinda wanchi kikamilifu.
Moja wa msemaji wa shirika linalo toa msaada kwa wakimbizi ( hakutoa jina) alisema " wanajeshi wa JM ya Kongo wanakuwa na wakati mgumu kutokana na kukusa mishahara na hata mishahara yenyewe ni midogo jambo jambo ambalo linawafanya kushindwa kutimiza swala la ulinzi wa raia na nchi.
"Vifaa vya kijeshi ambavyo wanatumia ni duni kulinganisha na vya kundi la upinzani linalo ongozwa na Bosco Ntaganda na wenzake ambao wanapingana na serikali ya Kinshasa inayongozwa na rais Joseph Kabila. 

Swala la Irani kuwa na nguvu za kinyuklia wa bado mvutano.

Baghdad, Iraq - 23/05/2012. Mkutano uliyo wakutanisha viongozi wa jumuiya ya kimataifa kutoka Ujerumani, China, Uingereza Urussi na Marekani wamekutana na viongozi wa Iran illikujadili kiundani kuhusu swala Iran kuwa na nyuklia.
Waziiri ambaye anashughurikia maswala ya nje ya nchi za jumjuiya ya Ulaya Catherine Ashton aliwakilisha muswada kwa viongozi wa Iran.
Hata hivyo shirika la habari la Iran IRNA limesema " muswada ambao umeletwa na Catherine Ashton hauna mageni na hauangalii faida za pande zote mbili na lazima ieleweke ya kuwa  pande zote mbili zifikie makubaliano ambayo yanafaida kwa nchi zote."
Iran imekuwa ikivutana na jumuiya ya kimataifa katika swala la haki ya nchi hiyo kuwa na uwezo wa nguvu za kinyuklia.

Muuguzi aliye husika katika kifo cha Osama bin Laden afungwa jela miaka 33.

Peshawar, Pakistan - 23/05/2012. Muuguzi ambaye alitoa uchunguzi wa kisayansi -DNA za aliyekuwa kiongozi mkuu wa kundi la Al Qaeda amehukumiwa kwend jela miaka 33.
Shakeel Afridi amakutwa na hatia ya kuhusika katika kufanya uhaini kwa kutoa habari za kisayansi ambazo nikinyume na sheria ya Pakistan
Mwezi January waziri wa ulinzi wa Marakani Leon Panetta alisibitisha kwa kusema " Afridi amekuwa mfanyakazi wa idara ya upelelezi ya Marekani CIA   kwa kutoa habari za kisayansi DNA ili kumjua na kumtambua aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda Osama bin Laden."
Shakeer Afridi alikuwa muuguzi wa kuheshimiwa na likamatwa wiki mbili baada ya kifo cha Osama bin Laden kufanywa na jeshi maalumu la Marekani.

Wamisri  wapiga kura  kumchagua rais wa nchi.

Kairo, Misri - 23/05/2012. Wananchi wa Misri wapiga kura leo ili kumchagua rais atakayeongoza nchi hiyo.
Uchaguzi huo wa rais wa Misri unafanyika kwa mara ya kwanza kushiriisha vyama vingi au uchaguzi wa kidemokrasia tangu kuangushwa kwa rais Husni Mubarak ambaye litawala Misri kwa miaka 30.
Viongozi wanaogombania uongozi wanatoka katika chama kinachojulikana Muslimu brothorhood, na viongozi ambao walikuwa wakati wa utawala wa rais Husni Mubarak.
Hamdy Abdel Salman ambaye ni mmoja ya mwakilishi wa Morsi alisme "  hadi kufikia sasa kila kitu kipo sawa japo kuwa watu walikuwa wanalalamika kuwepo kwa mistari mirefu."
Wanchi wa Misri anapiga kura  ili kupata kiongozi atakeye iongoza Misri kwa kufata misingi ya kidemokrasi baada ya miezi 15 kupita bila kuwa na serikali ya kudumu.

No comments: