Thursday, March 21, 2013

Baraka Obama Wapalestina na Waizrael lazima wafikilie upya ili amani iwepo.

Baraka Obama  Wapalestina na Waizrael lazima wafikilie upya ili amani iwepo.

Ramallah, Palestina - 21/03/2013. Rais wa Marekani amewataka viongozi wa Palestina na Izrael kukutana tena ili kuongelea swala la kuwepo na kuundwa taifa la Wapalestina litakalo pakana na Izrael.
Rais Baraka Obama akiongea kwenye mkutano  wa pamoja na waandishi wa habari, alisema "Inabidi viongizi wote lazima wafikilie upya ili kuweza kufanikisha kupatikana kwa amani kati ya Waizreal na Palestina na ni haki kwa Wapalestina kuwa na Taifa lao ili waweze kujenga maisha yao ya baadaye kwa kizazi kijacho."
Naye rais wa Wapalestina Mahamoud Abbas akichangia katika mkutano huo alisema " kikwazo kikubwa ni kuendelea kujengwa kwa makazi ya Kiyaudi katika eneo letu sisi Wapalestina na inabidi ujenzi huu usimamishwe na hali hii imekuwa ikipingwa na kulaaniwa na jumuiya ya kimataifa na hata umoja wa mataifa umesha piga kura zaidi ya mara 13 kupinga ujenzi huo."
"Hivyo ujenzi wa makazi lazima usimame ili kufanikisha mazungumzo na Waizrael."Alisema rais Abbas.
Ziara ya rais Obama katika eneo la Westbank ni ya kwanza tangu kuwa rais wa Marakani na kbla ya kuonana na viongozi wa Wapalestina aliongea kwanza na viongozi wa Izrael ambao walisisitiza nia yao ya kutaka mazungumzo ya amani kati yao na Wapalestina yaendelee.

1 comment:

Anonymous said...

My personal Tгο Ϲhοi liκewise ply уou with
аn soft way of entertainment. Keгmit the Frog is a him,
you Misρlасе pοintѕ.


mу ωeb blog - ampmcomputersinc.com