Tuesday, March 19, 2013

Kadinali Jorge Mario Bergoglio asimikwa rasmi na kuitwa Papa Fransisko.

Kadinali Jorge Mario Bergoglio asimikwa rasmi na kuitwa Papa Fransisko.

Vatican, Vatican City - 19/03/2013. Maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki, viongozi wa serikali na marais wameudhuria kusimikwa kwa Kadinali Jorge Mario Bergoglio kuwa mkuu wa Kanisa Katoliki duniani.
Kabla ya kuongoza misa Kadinali Jorge Mario Bergoglio 76, alisimikwa uongozi huo na kupewa cheo cha Upapa kwa jina alilo chagua la Fransisko na kuwa ni Papa wa kwanza kutoka katika bara la Amerika.
Papa Fransisko akiongea baada ya kusimikwa na kuongoza misa alisema " nawaomba  wale wote wenye madaraka   wawajibike vyema katika nyazifa zao za kiuchumi, siasa na kijamii ili tuweze kulinda na kujenga jamii bora na mazingira yake."
Papa Fransisko, amechuku jina la Fransisko wa Assis ambaye alikuwa mtoto wa tajiri, lakini aliamua kwenda kuishi  na watu masikini wakati wa karne ya 13, na hivyo Papa Fransisko kusisitiza ya kuwa kanisa ni kanisa la watu masikini.
Papa Fransisko ni mzaliwa wa Argentina.

Wazimbabwe wakubaliana katika kura ya muda wa urais.

Harare, Zimababwe - 19/03/2013. Wananchi wa Zimbabwe wamepitisha kwa wingi wa kura kuunga mkono sheria itakayo tumikika kumruhusu rais kuongoza nchi kwa mihula miwili ikiwa atachaguliwa baada ya kumaliza awamu ya kwanza.
95% ya watu walio piga kura walikubaliaana na sheria hiyo ambayo itaanza kutumika baada ya uchaguzi mkuu wa urais utakao tarajiwa kufanyika  mwaka huu mwezi wa Julai.

 Siraha za sumu zatumika katika vita nchini Syria. 

Damascus, Syria - 19/03/2012. Serikali ya Syria  imelaumu vikundi vinavyo pigana na serikali kwa kutumia siraha zenye sumu.
Msemaji wa serikali ya rais Bashar al Assad  alisema' wapiganaji wanaopigana naserikali wametumia siriha zenye sumu katika mji wa Aleppo."
Hata hivyo msemaji wa kundi linalo pigana na serikali alikanusha madai hayo kwa kusema " huu ni uzishi mtupu, na tunaamini jeshi la serikali limetumia mabomu aina ya scud ambayo huenda ya na sumu."
Kufuatia habari hizi serikali ya Urusi imeonya na kulaani na kusema  linabidi lichunguzwe ukweli wake kwani " ikiwa  siraha za sumu zimeanguka mikononi mwa wapiganaji basi hali inaweza kuwa mbaya zaidi."
Habari hizi za matumizi ya siraha za sumu zimekuja baada ya wapinzani wa serikali ya Syria kufanya uchaguzi na kumchagua Ghasssa Hitto, kuwa waziri mkuu wa serikali inayo pingana na rais Bashar al Assad katika uchaguzi uliyofanyika nchini Uturuki jijini Instambul.
Ghasssan Hitto ambaye alikuwa akiishi nchi Marekani amesema  " hakuna  majadiriano na serikali ya Bashar al Assad."
Syria ina limbikizo la siraha za sumu na za kinyuklia ambazo kama zikitumika katika vita hivi vya wenye kwa wenye huenda eneo zima la bara Arabu likawa katika hali mabaya. 

 Irak bado mabomu yalipuka na ni miaka 10 tangu kuangushwa kwa Saddam Hussein

Baghdad, Iraq - 19/03/2013. Watu zaidi ya 48 wamepoteza maisha yao na zaidi ya watu 120 kujeruhiwa vibaya, baada ya mfululizo wa mabomu kulipuka wakati Wairak wanatimiza miaka 10 tangu kuangushwa kwa Saddam Hussein.
Mashambulizi hayo ya mabomu ambayo yalitokea katika masoko, holetini nakwenye kituo cha basi katikati ya jiji la Badhdad kwenye eneo linalo kaliwa na  watu jamii ya Kishia.
Uvamizi nchini Irak uliongozwa na Marekani mwaka 2003/19, kwa madai ya kuwa Saddam Hussein alikuwa amelimbikiza siraha hatari za sumu ya kinyuklia.
Tony Blair ambaye alikuwa waziri mkuu wa Uingereza na aliye unga mkono na kushirikiana na serikali ya Marekani katika uvamizi nchini Irak amesema " hajutii uamuzi wake wa kushiriki katika kung'oa  Saddam Hussein madarakani kwani hata kama vuguvugu hili la mapinduzi inalo endelea katika bara la Waaraabu lingefenikiwa kumuondoa madarakani Saddam Hussein, basi ingekuwa ni tukio ambao linge jawa na majuto makubwa kwa jumuiya ya kimataifa kwa kuzingatia ni nini kinacho endelea nchini Syria,  ambapo rais Bashar al Assad anavyo wafanyia wananchi wake."
Vita vya kuivamika Irak vilipoteze maisha ya Wairak zaidi ya 100,000 na wengi kujeruhiwa na mali nyingi za Wairak kuharibika.

2 comments:

Anonymous said...

How do i create a personalized banner for any blogspot blog?


Here is my blog transvaginalmesh411.net

Anonymous said...

Just want to say your article is as amazing. The clarity in your publish is simply spectacular and i can suppose you are knowledgeable in this
subject. Well with your permission allow me to grab your feed to keep
updated with coming near near post. Thanks one million and please keep up the enjoyable work.


Also visit my webpage - bkk-lv-nw.de