Monday, March 18, 2013

Papa Fransis aombwa kutatua mgogoro wa Kisiwa cha Falkland.

Bosco Ntaganda ajisalimisha mikononi mwa ofisi za Kibalozi nchini Rwanda.

Kigali, Rwanda - 08/03/2013. Kiongozi wa kundi la waasi wanaopigana na serikali ya Kongo Kinshasa amejisalimisha katika ofisi za ubalozi za Marekani zilizopo nchini Rwanda.
Bosco Ntaganda ambaye anatafutwa na mahakama ya kimataifa tangu mwaka 2006,  ili kujibu kesi zidi yake, alijipeleka mwenyenyewe kwenye ofisi za ubalozi wa Marekani na kutaka apelekwe kwenya mahakama ya kimataifa.
Hapo awali habari kutoka serikali ya Kongo Kinshasa zilisema ya kuwa Bosco Ntaganda amekimbilia Rwanda baada ya kundi lake kuzidiwa nguvu na kundi la M23 ambalo pia linapingana na serikali ya Kinshasa.
Viktoria Nuland ambaye ni msemaji wa ubalozi wa Marekani nchi Rwanda alisema " Bosco Ntaganda amewasili katika ofisi zetu leo hasubuhi na ameomba apelekwe mahakama ya kimataifa ya iliyopo nchini Uhollanzi,
" Na sasa serikali ya Rwanda na Marekani kwa kushirikana na mahakama ya kimataifa iliyopo nchini Uhollanzi zipo katika mazingumzo  ili kukuamilisha maombi ya Bosco Ntaganda."
Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Louise Mushikiwabo kwa kuthibitisha kuwepo kwa Bosco Ntaganda   kwenye ubalozi wa Marekani alisema "serikal ya Rwanda bado inalishughulikia swala hilo na ni kweli Bosco Ntaganda yupo katika ubalozi wa Marekani,"
Bosco Ntaganda mwenye asili ya Kitutsi  na aliyejulikana kwa jina la "Teminata - Terminator "alijiunga na jeshi mwaka 1990 akiwa na miaka 17, na kujisalimisha huko kwakwe kunaleta maswali mengi hadi sasa.

Mahakama yaombwa kufuta kesi zidi ya Uhuru Kenyatta.
Hague, Uholanzi - 18/03/2013. Mwanasheria anayesimamia kesi inayo mkabili rais mchaguliwa wa nchi Kenya ameitaka mahakama ya kutetea haki za binadamu iliyopo nchi Uholanzi kufuta kezi zidi ya mteja wake.
Mwanasheria Stephen Kay, ameimbia mahakama ya kuwa "ikiwa shahidi huyo wanne na  ambaye alitoa maelezo tata kuhusu mteja wake Uhuru Kenyatta basi kesi hiyo ifutwe kwani ushahidi huo ni dhaifu."
" Na hata hivyo tunekosa uaminifu na ushahidi uliyopo, kwani ushahidi uliyo kuwepo zidi ya Muthaura hauna tofauti na Uhuru Kenyatta."  
Uhuru Kenyatta amechaguliwa kuwa rais wa Kenya hivi karibuni kufuatia uchaguzi mkuu uliyofanyika nchini humo japo ana kesi inayo mkabili katika makahama ya kimataifa ya makosa ya jinai iliyopo nchini Uholanzi.

 Papa Fransis aombwa kutatua mgogoro wa Kisiwa cha Falkland.

 Rome, Itali - 18/03/2013. Rais wa Argentina amemumba kiongozi mteule wa Kanisa katoliki duniani kusaidia kutafuata suruhisho la mgogoro wa Kisiwa cha Falkland ambacho kinagombaniwa Uingereza na Argentina.
Rais Cristina Fernandez Kirchner alisema " nimeongea na Papa Fransis asaidie kutatua mgogoro wa kisiwa cha Falkland.
"Kwani hali inavyo kwenda tunaweza kujikuta nguvu za kijeshi zikatumika tena," alioongezea rais Kirchner.
Mazungumzo kati ya Papa Fransis na rais Cristina Fernandez Kirchner yalichukua dakika 20 kabla ya kufanyika sherehe rasmi  ya kumsimika wadhifa kamali wa Upapa Jorge Mario Bergoglio 76 na kuwa Papa Fransis ambayo viongozi na marais watahudhuria hapo  kesho.
Papa Fransis ni mzaliwa wa Argentina, na kabla ya kuteuliwa kuwa Papa alikuwa  Kardinali wa jiji la  Bueno Aires
  
India na Itali zavutana kidiplomasia.

 India, New Delhi, - 18/03/2013. Jaji mkuu nchini India amekataa takwa ya kuwa balozi wa Itali nchini India ana sheria inayo mlinda kutokana madaraka aliyo nayo.

Jaji Altamas Kabir alisema " mahakama imekosa imani na serikali ya Itali kwa kitendo walichofanya cha kushindwa kutimiza agizo ambalo serikali mbili zilikubaliana."
Jibu hilo la mahakama limekuja baada ya balozo wa Itali nchini India, Daniel Mancini kukataliwa kuondoka nchini India kwa madai ubalozi wa Itali nchini India uliweka dhamana ya kuwa washutumiwa hao wa wawili wangerudi nchini India ili kujibu mashitaka yanayao wakabiri ya mauaji ya raia wa Waindia walioku wavuzi wa  samaki.
Balozi Mancini alichukua dhamana ya kuachiwa kwa raia hao wa Itali na kuhaidi watarudi ili kijibu mashita yao, lakini wakati ukipo fika wa raia hao wa Itali kurudi nchini India hawakufanya hivyo, jambo ambalo serikali ya India imesema ni kunyume na makubaliano na sheria zilizopo.

Viongozi wa Jumuiya ya Ulaya kuachia madaraka 2014

Brussels, Ubelgiji - 18/03/2013. Viongozi wakuu wawili wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya wametangaza kuchia madaraka yao ifikapo mwaka 2014.
Wakiongea kwa nyakati tofauti, Herman Van Rompuy 65, ambaye alisha wahi kuwa waziri mkuu wa Ubelgiji and Catherine Ashton 56, ambaye ni mwanachama wa chama cha Labour cha Uingereza walisema ya kuwa umefikia wakati wa kuwapa watu wengine nafasi kuongoza.
Viongozi hao ambao walichaguliwa kushika nyazifa hizo mwaka 2009, wamekuwa wakishirikiana katika harakati nyingi za kudumisha jumuiya ya Ulaya  ili kuhakikisha umoja huu unakuwa imara zaidi.

No comments: