Wednesday, March 13, 2013

Habemus Papam kwa waumini wa Kanisa Wakatoliki.

Habemus Papam  tamko rasmi la Makadinari. 
 
  
Kengere na moshi mweupe watokea na kuashiria ya kuwa waumini wa Kanisa Katoliki wapata Papa mpya.

Vatican City, Vatican - 13/03/2013. Kadinari Jorge Mariao Bergoglio 76 mzaliwa wa Argentina ameteuliwa kuwa mkuu wa kanisa Katoliki duniani.
Jorge Mario Bergoglio atajulikana kwa jina la Papa Fransis na kuwa mkuu wa kanisa Katoliki wa 266 na amekuwa ni Papa wa kwanza kutoka nje ya bara la Ulaya  tangu miaka 1000 kupita.
Papa Fransis akiongea kuwashukuru  waumini na wale wote walio husika katika kufanikiasha kuteuliwa kwake alisema "Nawashukuru sana kwa  Makadinari wezangu kwa kunichagua kutoka mbali na kunileta hapa na ninge waomba muniombe."

Makadinari walichukua siku mbili katika maombi na kufanikiwa kumchagua Papa Fransis.

No comments: