Thursday, March 14, 2013

Botswana yaiomba msamaha Kenya.

Botswana yaiomba msamaha Kenya.


Gaberone, Botswana - 14/03/2013. Waziri wa mambo ya nje wa Botswana ameomba msamahaa kwa rais aliyechaguliwa hivi karibuni nchini Kenya.
Pandu Skelemani aliomba msaahaa huo baada ya kusema " serikali ya Bostwana itamzuia kuingia nchi rais mtarajiwa wa Kenya Uhuru Kenya ikiwa hatashirikiana na mahakama ya kimataifa ICC Hague, iliyopo nchini Uhollanzi. "
Hapo awali  serikali ya Kenya ili ilaumu Botswana kwa kuingilia mambo ya serikali nyingine."
Waziri Skelemani alisema " naomba msamaha kwa watu wa Kenya kutokana na kauli yangu ya hapo awali na serikali zetu zitakuwa kwa ukaribu bila wasiwasi."
Botswana imesha wahi pia kutoa onyo kwa rais wa Sudan Omar al Bashir ya kuwa ikiwa ataingia nchini humo atakamatwa.

China wapata rais mpya.

Beijing, China - 14/03/2013. Bunge nchini China limememchagua Xi Jinping kuwa rais wa nchi hiyo.
Xi Jinping 59, ambaye hapo awali alikuwa amesha apishwa kuwa mkuu wa majeshi atakuwa na kofia mbili za kuongoza nchi.
Uchaguzi huo ambao ulifanywa na wabunge 3000, na kura tatu hazikupigwa.  
Rais huyo mpya wa China anatarajiwa kufanya ziara yake ya kwanza nchini Afrika ya Kusini ifikapo mwisho wa mwezi Machi.

 Rais wa Ufaransa ataka vikwazo viondolewe kwa wapinzani wa serikali ya Syria

Paris, Ufaransa - 14/03/2013. Rais wa Ufaransa, amezitaka nchi wanachamwa jumuiya ya Ulaya kutoa vikwazo vya siraha kwa wapiganaji wanao pingana na serikali ya Syria.
Rais Francois Hollande aliyasema haya saa chache baada ya waziri wa mambo ya nje Laurent Fabius kusisitiza hipo haja ya jumuiya ya Ulaya kuondoa vikwazo kwa wapiganaji wanao pingana na serikal ya rais Bashar al Assad.
Waziri Laurent Fabius alisema " njia iliyo bakia ni kuwapa siraha wapiganaji hao, ambapo kutasaidia kufikia suruhisho la kisisa, kwani serikali ya Syria imekuwa ikipewa siraha na Iran na Urusi" 
"Na Ufaransa na Uingereza zipo tiyari kuondoa vikwazo hivyo bili kupata ruhusa kutoka kwa nchi wanachama wa Ulaya."Aliongezea waziri Fabius.
Hata hiyo kauli hizo za viongozi hao wa Ufaransa zitakuwa na wakati mgumu kupenya kwenye vichwa vya nchi wanachama wa Ulaya, kwa kuzingatia Ujerumani imekuwa ikisita kuunga mkono uamuzi huo.

 Benjamin Netanyahu aunda serikali ya muungano.

Jerusalem, Izrael - 14/03/2013. Waziri mkuu wa Izrael amefikia makubaliano na chama cha upinzani ili kuunda serikali.
BenjaminTetanyahu chini ya chama chake cha Likud-Yisrael Beitenu amefikia makubaliano na chama cha Yeshi Atid na Hatnua na chama kingine cha Kiyahudi.
Kuundwa kwa serikali ya Izrael kumekuja baada ya wiki tano kupita kufuatia uchaguzi mkuu uliyonfayika mwezi January 22, ambapo chama cha waziri mkuu Netanyahu hakikuweza kupata kura za kumwezesha kuunda serikali bili chama wapinzani.
Serikali ya Izrael imeundwa wakati rais wa Marekani Baraka Obama anatarajiwa kufanya ziara nchi Izrael.

1 comment:

Anonymous said...

Greetings! Quick question that's completely off topic. Do
you know how to make your site mobile friendly? My website
looks weird when viewing from my iphone4.
I'm trying to find a theme or plugin that might be able to fix
this issue. If you have any recommendations, please share.
Thank you!

Here is my webpage - View my web page
my website - View My web page