Wednesday, March 27, 2013

Makubaliono ya kuundwa benki ya nchi za BRICS bado kufikiwa.

Makubaliono ya kuundwa benki ya nchi za BRICS bado kufikiwa.

Durban, Afrika ya Kusini - 27/03/2013.Viongozi wa nchi zinazo kua kiuchumi duniani wamekutana nchini Afrika ya Kusini ili kuangalia ni kwa kiasi gani nchi hizo zitashirikiana katika kukuza uchumi.
Viongozi wa nchi hizo zinazo julikana kama BRICS ambazo zinajumuisha nchi za Brazil, Urusi, India, China na Afrika ya Kusini wamekutana na kujadili  muundo wa benki ya nchi hizo na itakavyo weza  kushindana na mabenki ya nchi za Ulaya Magharibi ambazo zimekuwa zikitawala mfumo wa fedha wa dunia.
Katika kikao hicho, viongozi hao hawakufikia muafaka kamili juu  kuundwa kwa benki yao na kukubaliana kutoa muda wa kuliangalia swala hilo kiundani.
Mwenyekiti wa kikao hicho, rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma alisema " tunayo matumaini ya kuunda benki hiyo na kwa sasa ni wajibu wa viongozi kwenda kukaa, kupanga na kuliangalia jambo hili kiundani ili kulifanikisha."
Benki hiyo ambayo inatarajiwa kuhitaji pesa za euro billioni 50, ambazo zitachangwa na nchi hizo za BRICS ili benki hiyo iweze kufanya kazi kikamilifu.
Viongozi hao walikutana ili kutimiza mazungumzo yaliyo fanyika nchini India New Dheli, mwaka mmoja uliyo pita ambapo  azimio la kuundwa kwa benki hiyo  lilijadiliwa.

Korea ya Kaskazini yazidisha uhasama na Korea ya Kusini.

Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 27/03/2013. Serikali ya Korea ya Kaskazini imesimamisha mawasiliano ya aina zote  kati yake na serikali ya Korea ya Kusini.
Uhasama huo kati ya nchi hizi mbili umekuja baada ya Korea ya Kusini kuendelea kufanya mazoezi ya kijeshi na Marekani, jambo ambalo Korea ya Kaskazini imelitaja ya kuwa ni la kutishia usalama wake.
Habari kutoka Korea ya Kaskazini zilisema "kutokana na hali iliyopo tunaona  vita vinaweza kutokea muda wowote na hivyo kuanzia sasa mawasilino ya aina yoyote na Korea ya Kusini hayatakuwepo."
Msemaji wa serikali ya Marekani amesema "hiki ni kitendo ambacho hakitaijenga serikali ya Korea ya Kaskazini, na inabidi serikali ya nchi hiyo iangalie kama vitendo inavyo fanya ni sawa na havitasaidia katika kuleta uimara wa usalama katika eneo zima la Peninsula."
Korea ya Kaskazini imekuwa ikitishia kuishambulia Marekani na kusema ya kuwa kitendo cha kufanya mazoezi ya kijeshi kwenye Korea Peninsula kumevunja mkataba  uliyo wekwa wa vita wa mwaka 1950-53.

Sheria ya mlinda Abuu Qatada nchini Uingereza.

London, Uingereza - 27/03/2013.  Mahakama ya rufaa ya Uingereza imelitupilia mbali ombii la serikali  ya Uingereza la kutaka muhubiri maarufu wa dini ya Kiislaam arudishwe nchini kwao.
Abuu Qatada ambaye ni raia wa Jordan ameruhusiwa na mahakama ya Uingereza kuendelea kuishi nchini humo, japo serikali ya Uingereza kupitia ombi la waziri wa mambo ya ndani ya nchi hiyo Thereza May kutaka Abuu Qatada kuondolewa nchi Uingereza kwa madai anahatarisha usalama wa nchi.
Jopo la majaji wa mahakama ya rufaa lilitoa hukumu kwa kusema "hakuna ushahidi wa kutosha ya kuwa kesi inayo mkabili  Abuu Qatada nchini Jordani itaendeshwa kwa kufuata sheria na haki za binadamu."
Kufuatia uamuzi huo wa mahakama, waziri kimvuli wa mambo ya ndani, Yvette Cooper alisema " hii inasikitisha saana, na waziri Thereza anatakiwa kutumia kila sheria ili kufanikisha kuondelewa nchi kwa Abuu Qatada."
Abuu Qatada ambaye ni raia wa Jordan aliomba hifadhi nchi Uingereza mwaka 1993, baada ya jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Jordan kushindwa, na mwaka 1999 alikutwa na hatia  kwa kosa la uhaini nchini Jordan, baada ya kesi kuendelea japo hakuwepo nchini humo.

2 comments:

Anonymous said...

Why users still use to read news papers when in this technological globe
all is existing on web?

Feel free to surf to my homepage http://wiki.main.de/w/index.php?title=Benutzer:JenniDunn

Anonymous said...

Τhіѕ will cheсκ chat and Cause populаrіty of the onlіne
gаmеs arе numerοus. Mаny of
the οnline gameѕ eаrmark for preschoοlers аre
eduсational, theу're a Release Multiplayer On the web game, based on the True Mafia lifestyle so called "La Cosa Nostra".