Tuesday, March 5, 2013

Rais wa Venezuela Hugo Chavez aaga dunia.

Rais wa Venezuela Hugo Chavez aaga dunia.


Karakas, Venezuela - 05/03/2012. Rais wa Venezuela Hugo Chavez amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na ugonjwa wa saratani.
Akitangaza kifo cha rais Hugo Chavezi, makamu wa rais wa Venezuela Nikolas Maduro alisema" Wanachi wenzangu na marafiki wa Venezuela, rais wetu mpigania haki na mwanamapinduzi Hugo Chavez amefariki dunia.
Maadui wa Hugo Chavez walimpandikiza viini vya ugonjwa wa saratani., ambavyo vimeyaondoa maisha yake." 
Marehemu rais Hugo Chavez 58, amekuwa akisumbuliwa na ugonjwa huo wa saratani, na alikuwa akifanyiwa matibabu nchi Kuba.
 Hugo Chavez ametawala nchi Venezuela kwa muda wa miaka 14 na alikuwa amechaguliwa kuiongoza Venezuela baada ya kufanyika uchaguzi mkuu hivi karibuni nchini humo,lakini kushindwa kuhudhulia sherehe ya kuwapishwa kwake kama rais kwani alikuwa katika matibabu nchini Kuba..
Kufuatia kifo cha rais Hugo Chavez, serikali ya Venezuela imewafukuza maafisa wa kijeshi wa Marekani kwa kuwapa masaa 24 kuondoka nchini Venezuela.
Kabla ya kifo cha rais Chavez, Venezuela na Marekani zilikuwa hazina uhusiano mzuri.

  Netanyahu ataka mbinu mpya kwa Iran.


 New York, Marekani -05/03/2013.Waziri mku wa Izrael ametahadharisha Marekani na washiriki wake ya kuwa Iran ipo inakaribia kuvuka mstari mwekundu katika harakati zake za  sayansi ya kinyuklia.
Benjamin Netanyahu akihutubia katika mkutano kwa kupitia mtandao kwa wajumbe wa ushirikiano wa Izrael na Marekani (American Izrael Public Affairs Committee - AIPAC) alisema. "vikwazo zidi ya Iran havifanyi kazi na Iran ipo inaendelea na mpango wake wa kutengeneza siraha za kimyuklia jambo ambalo ni la hatari kwa nchi majirani zake  na eneo zima la ukanda wa mashariki ya kati.
 "Inabidi hatua nyingine ziangaliwe ili kuizuia Iran na mpango wake wa kuendelea na uzalishaji wa nyuklia."
Mkutano wa AIPAC ni mkutano ambao huwakutanisha wajumbe wa Marekani na Izrael ili kujadili ni kwa jinsi gani watashirikiana kwa ukaribu ili kudumisha umoja wao.

Uhuru Kenyatta aongoza katika uchaguzi wa urais.

Nairobi, Kenya - 05/03/2013. Mgombea wa kiti cha urais wa Kenya, Uhuru Kenyatta anaongoza katika  kura zidi ya mpinzani wake Raila Odinga.
Uhuru Kenyatta ambaye mpaka sasa anaongoza kwa asilimia 53% za kura zidi ya mpinza  wake Raila Odinga ambaye mpaka sasa amepata asilimia 42% za kura na huku kura nyingine bado zinahesabiwa.
Hata hivyo mkuu wa kamati ya uchaguzi mkuu amesema "bado kuna baadhi ya majimbo yanasubiriwa ili kuweza kupata idadi kamili ya kura zote."
"Napenda kuwataka Wakenya wote wawe na subira." 
Uchaguzi mkuu wa kumchagua rais na wabunge nchini Kenya umekuwa ukingaliwa kwa makini na jumuiya ya kimataifa , hii inataokana na vurugu zilizo tokea mwaka 2007-8 baada ya uchaguzi mkuu wa urais kufanyika ambapo watu zaidi ya 1000 walipoteza maisha.  




2 comments:

Nifty Tips said...

In this stock market blog share market investors and day traders will get

clear view for the Nifty Tips, stocks and various In this stock market blog share

market investors and day traders will get clear view for the Commodity

Tips
, stocks and various commodities along with the daily stock market

opening trend. This blog covers NSE, BSE,MCX and NCDEX completely.

Anonymous said...

Εxсeptionаl ρoѕt but I wаs wondering if уou
cοuld wrіte а littе more οn thіs subjеct?
I'd be very grateful if you could elaborate a little bit further. Appreciate it!

Also visit my site - Dien thoai