Nelson Rolihlahla Mandela aombewa na maelfu.
Johannesburg, Afrika ya Kusini - 10/12/2013. Viongozi kutoka nchi 91, marais, wakuu wa nchi, na maelfu ya watu, wameudhuria ibada ya maombolezi ya kumwaaga aliyekuwa rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela ambaye alifariki ya tarehe 05/12/2013 huku akiwa na umri wa miaka 95.
Viongozi mbali mbali walitoa hotuba zao za mwisho kwa Nelson Mandela ikiwa ni ishara ya kukubali kwao kuwa yote aliyo simamia Nelson Mandela yalikuwa ni ya haki na kukubalika katika harakati zake za kupigania kuung'oa utawala wa kibaguzi wa Makaburu.
Akiongea rais wa Afrika ya Kusini, Jacob Zuma alisema "Nelson Mandela - Madiba alikuwa mtu wa aina yake na hakuna mwingine atakaye kuwa kama Madiba."
Naye rais wa Marekani Baraka Obama akihutubia katika siku ya kumuuga Nelson Mandela alisema" Hatuta mwona tena Nelson Mandela.
Mandela ulikuwa mtu wa watu na tunakushukuru kwa kila jambo ulilofanya, ulikuwa unampenda kila mtu, na wala ukujali rangi yake au wapi alitokea na umetuachia kumbukumbu kubwa na tumejifunza mengi toka kwako."
Ili kuthibitisha aliyo simamia Nelson Mandela ya kumpendana na maadui zetu na ndiyo njia pekee ya kufikia kuwepo na amani kwa maasimu wa kubwa wa kisiasa wa kihistoria ni pale rais wa Baraka Obama alipo peana mkono na rais wa Kuba Raul Castro wakati alipo wasili kwenye jukwaa la tayari kwa kuanza misa rasmi ya maombelezi ya rais wa kwanza Mwafrika mweusi Nelson Mandela.
Wajane, Winnie Mandela na Graca Machel wakiwa wamekaa kwa huzuni katika misa ya maombelezi ya mume wao Nelson Mandela na picha ya chini wakipusiana kabla ya kukaa tayari kwa misa.
Mwili wa Neslon Mandela utawekwa katika jengo kuu la serikali - Union Bulding kwa siku tatu, kwa ajili ya watu kumwaga kwa mara mwisho kabla ya kuhifadhiwa katika kijiji alichokulia Qunu siku ya tarehe 15/12/2013.
No comments:
Post a Comment