Wednesday, December 11, 2013

Wezi wavunja nyumba ya Askofu wakati yupo kwenye misa ya Nelson Mandela.

Papa Fransis achaguliwa kuwa mtu muhimu wa mwaka 2013.

Vacan City, Vatican - 11/12/2013. Papa Fransis amechaguliwa kuwa mtu muhimu duniani na  gazeti la Time na kuwashinda Edward Snowden na rais wa  Syria Bashar Al Assad.

Akieleza uamuzi wa kumchagua Papa Fransis kuwa mtu muhimu katika msimu wa mwaka 2013, mhariri mkuu Nancy Gibbs amesema "Katika kipindi cha miaka 1200 Papa Fransis ni kiongozi wa kwanza kutoka Amerika kuongoza kanisa kubwa duniani na ameonyesha uwezo wake na hasa katika kubadirisha mwenendo  wa kanisa Katoliki."

Papa Fransis  amekuwa kiongozi wa tatu wa kanisa Katoliki kuteuliwa kwa kufuata nyayo za Papa John XXII mwaka 1962 na Papa John Paul II 1994.


Wezi wavunja nyumba ya Askofu wakati yupo kwenye misa ya Nelson Mandela.
 
Cape Town, Afrika ya Kusini - 11/12/2013. Wezi wamevunja na kuingia kwenye nyumba ya Askofu Mkuu Mstaafu  wa Kanisa la Anglikani  jiji Cape Town.

Tukio hilo limetokea wakati Askofu Desmond Tutu 82 na mkewe walipokuwa wamekwenda jijini Johannesburg kuhuria misa ya kumkumbuka ya marehemu  rais Nelson Mandel ambaye alikuwa rais wa kwanza  mweusi wa Afrika ya Kusini tangu kuangushwa kwa utawala wa ubaguzi wa rang


Mwangalizi na msimamizi wa Askofu Tutu Roger Friedman alisema" nyumba ya Askofu imevunjwa na mpaka sasa hatuwezi kusema ni vitu kiasi gani vimeibiwa "

Hii itakuwa ni mara pili kuvunjwa kwa  nyumba kwani mara ya kwanza ilivunjwa Agosti 7/2013, ambapo wezi waliingia nakuchukua baadhi ya vitu huku Askofu Desmond Tutu akiwa amelala na mkewe ndani.

Askofu Desmond Tutu 82 ni mshindi wa Nobel ya Amani ya mwaka 1984.

No comments: