Sunday, December 15, 2013

Nelson Rolihlahla Mandela apumzishwa kwenya makao yake ya milele.

Nelson Rolihlahla Mandela apumzishwa kwenya makao yake ya milele.




Qunu, Umthatha,  15/12/2013. Nelson Rolilhalha Mandela - Madiba kiongozi na rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini huru amepumzishwa kwa amani katika makao yake ya milele kwenye kijiji alicho kulia na kucheza wakati wa udogo na ujana wake.

Kijiji cha  Qunu, kijiji ambacho Nelson Mandela amelazwa na  huku  misa ya kumuaga ilifanyika kwa muda wa masaa mawili,wakati ndugu wa karibu, jamaa, machifu wa ukoo wa Nelson Mandela, viongozi tofauti kutoka sehemu mbalimbali dunia, na marafiki zake wakaribu walishuhudia kupumzishwa kwa Madiba.

Nelson Rolihlahla Mandela 95, kabla ya kushushwa kwenye makao yake ya  milele, aliaagwa kwa kupigiwa mizinga 21 ikiwa ni ishara ya kumuaga kama kiongozi na rais wa nchi.


Na kwa sasa Nelson Rolihlalha Mandela - Madiba hatupo naye kimwili, ila kiroho tupo naye na mishumaa 95 iliyo washwa ikiwa ni ishara ya kuwa miaka 95 aliyo ishi bado tupo naye daima, Amin.

Amba Kahle Utata, Umkhulu, Nelson Rolihlahla Mandela - Madiba.


No comments: