Wednesday, December 18, 2013

Angela Markel kuonngoza Ujerumani kwa mara ya tatu.
 
 
Berin, Ujerumani - 18/12/2013. Angela Markel 59, ameapishwa tena kwa mara ya tatu kuwa Kasela wa Ujerumani na kupewa madaraka ya kuiongoza nchi hiyo ambayo ni uti wa mgongo katika jumuiya wa nchi wanachama wa muungano wa Ulaya.
Kuapishwa kwa Angela Markel kumekuja baada  ya kufikia makubaliano ya chama chake cha CDU  na chama chenye mrengo wa kati kushoto cha SPD ambapo kwa pamoja wataunda serikali ya muungano itakayo iongoza Ujerumani.
 
Angel Markel amekuwa kiongozi wa kwanza kushinda uchakuzi nakuwa kansela tangu vita vya pili vya dunia chini ya chama chake cha CDU ( Christian Democratic Union).
 
Kufuatia kuapishwa kwa Angela Markel kuwa  Kansela wa Ujerumani, wanchi wa Ujerumani wanatongezewa kima cha chini cha mshahara  kama ahaadi ambazo zili aidiwa wakati wa kampeni.
 
  
Baada ya mapinduzi kushindwa hali ya hatari yatangazwa chini Sudani Kusini.
 
Juba, Sudani ya Kusini - 18/12/2013. Milio ya risasi imekuwa ikisika katika jiji la Juba na wanajeshi wanao muunga mkono rais wa sasa Sudani ya Kusini Salva Kiir kuvamia makazi ya makamu wa rais wa nchi hiyo ambaye anasadikiwa kuwa kiongozi wa kutaka kupindua serikali ya Kiir.
 
 Hadi kufikia sasa  watu  zaidi ya 500 waliopoteza maisha kutokana na mashabulizi ya kukusudiwa ya kuaangusha serikali ya rais Kiir na watu  wengine zaidi ya 20,000 kukimbilia katika eneo lenye makazi ya  ofisi za Umoja wa matafa nchi Sudani ya Kusini.
 
Kufuatia jaribio la kuipindua serikali, makamu wa rais Riek Machar ameshutumiwa kuwa muhusika mkuu baada ya kufukuzwa kazi na rais Kiir na baadhi ya watu kukamatwa na kupigwa marufuku matembezi ya usiku hadi hapo hali itakapo kuwa shwari.
 
Riek Machar alitangaza kuwa anataka kugombea urais wa wakati wa uchaguzi wa urais wa mwaka 2015, na alitoa kauli ya " nchi aiwezi kutawaliwa na udikteta wa utawala wa mtu mmoja."na bado hajakamtwa wala alipo hapajulikani.
 
Sudani ya Kusini imekuwa na msuguano wa kisiasa wa ndani tangu kupata uhuru wake toka  Sudan 2011.
 
Jela miaka minne na bakora juu.
 
Riyadh, Saudi Arabia - 18/13/2013. Mwanaharakati nchi Saudi Arabia amehukumiwa kupigwa viboko 300 na kifungo cha miaka 4 kwa baada ya kukutwa na hatia ya kupinga sharia zilizo wekwa na serikali ya  ufalme wa nchi hiyo.
 
Omar al Saed 24, ambaye kesi yake ilisikilizwa katika mahakama ya ndani na kukataliwa kuwa na mwanasheria wa kumtete  nabaadaye  kukutwa na kosa la kuikosoa serikali ya  kifalme ya Saudi Arabia kwa kukiuka  haki za binadamu na
 
Saudi Arabi ni moja ya nchi tano ambazo zimekuwa zikishutumiwa na shirika la kutetea haki za binadamu la Amnest International kwa kukiuka haki za binadamu. 
 
 
Urusi yazidi kutanua nguvu za mabawa yake
 
 
Moscow, Urusi - 18/12/2013. Serikali ya Urusi na serikali ya Ukraini  zimekubaliana kibiashara na kiuchumi, baada ya viongozi wa nchi hizo mbili kukutana jiji Moscow.

Rais wa Urusi Vladmir Putin na rais wa UkrainiVictor Yanukovich walikubaliana kushirikiana kwa ukaribu kati ya nchi hizo katika masuala ya kibiashara, kiuchumi na kisiasa, ambapo Urusi ilikubali kushusha bei ya gesi na mafuta kwa nchi ya Ukraini na kutoa kiasi cha $ dola za Kimarekani 15 billion kwa Ukraini ili iliweze kujenga uchumi wa nchi yake.

Akiongezea baada ya makubaliano hayo rais Putini alisema "makubaliano ya leo ni ya hiyari kati ya nchi hizi mbili na Urusi itachangia pia kwa kiasi kikubwa katika masuala ya kiulinzi nchi Ukraini"

Makubaliano hayo yamekuja wakati wanachi wa Ukraini wakiwa wamegawanyika,  baaadhi yao kutaka nchi yao ijihusishe zaidi na nchi za jumuiya ya muunganao wa Ulaya (EU), na wa wengingene wakitaka nchi hiyo kuwa karibu na Urusi, jambo ambalo limesababisha maandamano makubwa katika jiji la Kiev na kwenye baadhi ya mikoa nchini humo.

Kufuatia makubaliano hayo kati ya Urusi na Ukraini, viongozi wa vyama vya upinzani nchi Ukraini wamedai yakuwa kitendo cha rais Yanukovich kukubaliana na Urusi ni kuvunja nia ya nchi hiyo kuwa mwanachama wa nchi za muungano wa umoja wa Ulaya,  ambao baadhi ya Waukraini wanahisi kutawarahisishia kuwa karibu na nchi hizo za umoja wa Ulaya.

No comments: