Friday, December 27, 2013

Rais wa Sudan ya Kusini akubali suruhu.

Rais wa Sudan ya  Kusini akubali suruhu.

Juba, Sudan ya Kusini - 27/12/2013. Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir  amekubali kusimamishwa mapambano ya kivita kati yake na kundi ambalo linaunga mkono mpinzani wake Riek Machar ambaye alikuwa makamu wake wa urais.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya  na waziri mkuu wa Ethiopia  Hailemariam Desalegn waliweza  kumshawishi rais Kiir kukubali kusimamishwa kwa vita baada ya kukutana na kujadiliana katika mji mku  wa Juba.

Akiongea  baada ya rais Kiir  kukubali kusimamishwa kwa vita , rais Uhuru Kenyatta amaesema " nimefurahishwa na kitendo cha rais Kiir kukubali kusimamisha vita, kwani nafasi iliyopo ni finyu, na naomba ijulikane kuwa  IGAD haitaruhusu kuona rais aliyechaguliwa kihalali anatolewa madarakani kwa nguvu"

" Na nawaomba Riek Machar na rais Salva Kiir  kuhakikisha amani inarudi nchini Sudani ya Kusini kwani vita siyo suruhu ya kuleta maendeleo ya nchi." Aliongeza  rais Uhuru Kenyatta.

Jitihada za kusimamisha vita nchini Sudan ya Kusini  zinasimamiwa na  (Inter-Government Authority on Develoment -IGAD) ikiwa  na nia ya kusimamia uongozi bora na kuhakikisha kuondoa migogoro ya kisiasa katika nchi zilizopo  Afrika ya Mashariki na Kati.

Mvutano kati ya Udugu wa Kiislam na serikali waiweka amani ya Misri njia panda.


Kairo, Misri -27/12/2013. Waandamaji wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam ( Muslim Brotherhood) wamepambana polisi katika matukio tofauti yaliyo tokea nchi Misri tangu kutangazwa kuwa kudi hilo ni kundi la kigaidi nchi Misri.

Katika maandamano hayo watu watatu wamepoteza maisha jiji Kairo, na wengine kujeruhiwa vibaya wakati polisi wa kuzuia ghasia  walipo pambana na waandamanaji,  na zaidi ya watu 265 wamekamatwa kutokana na vurugu hizo,  

Tangu kutolewa madarakani kwa nguvu kwa rais Mohammed Morsi, hali ya amani na utulivu imechafuka nchini Misri, na hii inatokana na wanachama  wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam kutaka rais Mohammed Morsi arudishwe madarakani na pia wanapinga kitendo cha serikali kukitangaza cha chama cha Udugu wa Kislaamu kuwa cha kigaidi.

Saada al Hariri alia na Hezbollah.

Beiruti, Lebanon - 27/12/2013.  Saad al Hariri ambaye alisha wahi kuwa waziri mkuu wa Lebanoni, amelilaumu kundi la Hezbollah kwa kuhusikia na shambulizi la bomu ambalo limemuua mmoja ya mshauri wake mkuu.

Mohamad Bahaa Chatah 62, aliuwawa baada bomu kulipuka  katikati ya msafara wake wakati  alipo karibia ofisi za majengo ya serikali ambapo alikuwa njiani keelelea kwenye mkutano wa kuipinga Syria uliyokuwa ukiongozwa na Saad al Hariri

Mlipuko huo pia uliharibu majengo na kusababisha baadhi kushika moto na kuungua vibaya.

Akiongea kuhusu mauaji ya Chatah, Saada al Hariri alisema " watu walio muua Chatah ni wale ambao wanataka haki isitendeke kufuatia kuwepo na kesi inayotarajiwa kuanza kwenye koti ya kimataifa mjini  Hague Uholanzi mapema mwezi January 2014."

Mohamad Chatah, alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali ya Syria,  amekuwa akipinga na kulaumu kundi la Hezbollah kwa kushirikiana na rais Bashar al Assad katika vita vinavyo endelea nchi Syria.

Kifo cha Chatah kimekuja wiki tatu kabla ya kuanza kesi zidi ya baadhi ya wanachama wa Hezbullah ambao wanasadikiwa kuhusika katika mauaji ya  mwaka 2005 ya waziri mkuu wa Lebanoni  Rafik al Hariri ambaye ni baba wa Saad al Hariri,



1 comment:

Anonymous said...

http://pay4shares.com/?share=111024