Saturday, December 7, 2013

Nelson Rolihlahla Mandela atutoka na hatupo naye kimwili.

Afrika yampoteza shujaa mwingine.


Pretoria, Afrika ya Kusini - 07/12/2013. Ulimwengu mzima upo katika  maombelezi ya kifo cha  Nelson Mandela 95, kiongozi mashuhuri aliyeingia katika madaftari ya historia ya karne ya 20.



Enzi za ujana wa Nelson Rolihlahla Mandela.

 Serikali duniani kote  zimeshushwa bendere za nchi zao nusu milingoti ikiwa ni ishara ya  maombolezi  baada ya rais  wa kwanza Mwanaafrika Nelson Rolihlahla  Mandela - Madiba kutangazwa kuwa ameaaga dunia.  

Kufuatia kifo chake, viongozi wa kimataifa wameelezea masikitiko yao na kusifu mchango wake wakati wa uhai wake na jinsi alivyo weza kupambana na ubaguzi wa rangi na mtu aliyekuwa akipigania haki, uhuru na usawa.
Nelson Mandela baada ya kuachiwa huru akiwa na mkewe Winnie Madikizela Mandela.


Ahaahaaa "Rolihlahla, usiwaambie kitu, tuonyeshe vitendo"Hapa anaoekana hayati Nelson Mandela akiwa na mkewe Winnie Mandela  siku kadhaa baada ya Nelson Mandela kutoka gelezani ambapo alikaa jela miaka 27 na Winnie Mandela alikuwa imara katika hali na mali kuendeleza harakati za kumuunga mumewe huku akitunza watoto wao.

Wakiongea kwa nyakati tofati.

Rais Barack Obama wa Marekani amesema kwa kufariki dunia Nelson Mandela " ulimwengu umempoteza mmojawapo wa binaadam mwenye ushawishi mkubwa kabisa, mwenye moyo wa kijasiri kupita kiasi na mwenye imani kupita kiasi. 

Akinukuu  aliyosema wakati  Mandela anahukumiwa  kwende jela maisha, rais Obama 
"Madiba alipofikishwa mahakamani mwaka 1964  alisema nimepigana dhidi ya utawala wa kimabavu wa waupe na nimepigana dhidi ya utawala wa kimabavu wa watu weusi. napiganiamaadili ya kuwepo jamii huru na ya kidemokrasia ambapo watu wote wataishi pamoja kwa furaha na kuwa na fursa sawa  na pia ni  maadili ninayotaraji kuyaendeleza maishani mwangu na ikihitajika, basi pi niko tayari kufa kwa ajili ya maadili hayo."

Naye rais wa Brazil Dilma Roussel amemtaja Nelson Mandela kuwa  "mtu mashuhuri mwenye ushawishi mkubwa kabisa wa karne ya 20 na  ameongoza utaratibu wa maendeleo katika historia ya binaadam kwa busara na mapenzi ,  utaratibu uliopelekea kumalizika kwa ubaguzi wa rangi na mtengano nchini Afrika ya Kusini"
Nelson Mandela akiwa jela katika kisiwa cha Roben kilichopo katika bahari ya Atlantiki karibu na jiji la Cape Town - Afrika ya Kusini.


Malkia Eliabeth wa pili wa Uingereza pia ameelezea masikito yake kutokana na kifo cha Nelson Mandela akisifu juhudi za Nelson Mandela nakusema  "Juhudi zake ndizo zilizopelekea kuwepo Afrika kusini yenye amani hii leo."
Baadi ya viongozi ambao walikuwa na urafiki wa karibu na Nelson Mandela.


Enzi za uhai wao, Nelson Mandela akiwa na rais wa kwanza wa Tanzania Julius Nyerere ambaye serikali yake ilichangia kwa kiasi kikubwa  katika  vita ya kuuong'oa utawala wa  serikali ya Kikaburu ya  Afrika ya Kusini.


"Comredi karibu" haya ndo maeneo aliyosema Hayati Nelson Mandela wakati akimkaribisha rais wa Kuba Fidel Castro.

Nelson Mandela alikuwa mtu wa shukurani, hapa anaonekana akiwa na kiongozi wa Libya hayati Muammar Gaddafi wakati alipo kwenda kumwona japo dunia ilimtenga Gaddafi.


Hadi kukutwa na umauti, Nelson Mandela na Robert Mugabe urafiki wao ulikuwa waukaribu, hapa wanaonekana wakibadirishana mawazo wakati viongozi hawa walipo kutana, enzi za uhai wa Nelson Mandela.
Kila mpigania  haki za binadamu mabdela alikuwa rafiki ya Mandela. Hapa Hayati Yasir Arafat na Hayati Nelson Mandela enzi za uhahi wao walipokutana.

Hayati Nelson Mandela  alizaliwa July 18/ 1918 na kufariki Desemba 05/ 2013 anatarajiwa kupunzishwa 15/12/2013, hii ni kwamujibu wa serikali ya Afrika ya Kusini.


No comments: