Tuesday, December 31, 2013

Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu mfululizo.


Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu  mfululizo.

Moscow. Urussi - 31/12/2013. Muuaji ya kigaidi yametolea tena kwa mara ya pili katika mji wa Volgograd na kuuwa watu wapatao 14 na wengi 41 kujeruhiwa vibaya ja.

Mauji hayo yalitokea baada ya  bomu kulipuka katika basi la abiria linalo fanya mizinguko ya kuchukua abiria katika mji huo na kuwashitua wananchi wengi wa Urussi ambapo nchi yao ipo mbioni kuandaa mashindano ya michezo ya Olympic Baridi siku chache zijazo.

Mlipuko wa bomu  ndani ya basi umefuatia mlipuko mwingine ambao umetokea siku moja katika kituo cha treni cha mji huo na kusababisha vifo vya watu 18 na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya baada ya muuaji wa kujitolea muhanga kusimamishwa katika kizuizi cha kuingilia katika kituo hicho.

Kufuatia milipuko hiyo katika mji wa Volgograd, rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza ulinzi uongezwe na kuhaidi kuwa wale wote ambao wanahusika na milipuko hiyo ambayo ina nia ya kutishia wananchi wa Urusi watatiwa nguvuni na sheria itapitisha panga lake kwao.

No comments: