Serikali ya Marekani yaruhusiwa kukupo.

Washington, Marekani 03/08/2011. Bunge nchini Marekani limepitisha muswada kwa serikali kuweza kukopa jambo ambalo lilikuwa linatishia uchumi wanchi na hasa wafanyakazi waserikali.
Kura zilizo kubali mswada huo ni 74 na zilizo kataa 26 na mswada huo ulikuwa unahitaji kura 60 ili uweze kupitishwa.
Kufuatia kupitishwa muswada huo, rais wa Marekani Baraka Obama amesaini muswada huo, ili kuiwezesha serikali kuweza kukopa kwa ajili ya kuendesha shughuli zake na hasa kuweza kulipa mishahara ya wafanyakazi wake.
Hata hivyo wataalamu wa mambo ya uchumi wanadai yakuwa muswada huo hautakuwa jibu la kutatua matatizo ya kiuchumi nchini humo kwa kipindi kirefu kijacho.
Serikali ya Marekani ilikuwa inasubiri muswada huo kupitishwa, jambo ambalo kama muswada huo usingepita siku ya Jumanne 03/08/2011, uchumi wa nchi hiyo ungekuwa katika hali mbaya na kuathiri duniani kote.
Hosni Mubaraka afikishwa mahakama kujibu mashitaka zidi yake.


Hosni Mubaraka , watoto wake na viongozi waliohusishwa katika kesi hizo waliwasilishwa katika mahakama iliyopo jijini Kairo huku maelfu ya wanchi wakingoja kwa hamu kuona jinsi kesi hiyo itakavyo endeshwa.
Hosni Mubaraka aliwasilishwa kwa ndege kutokea mji wa Sharm el Sheikh ambako andipo anapoishi tangu kutolewa madarakani miezi sita iliyopita na nguvu zawananchi.
Hata hivyo Hosni Mubara ambaye anasumbuliwa na magonjwa aliwasili akiwa kwenye kitanda cha kubebea wagonjwa ili kusikia kesi zidi yake.
Kesi zidi ya kiongozi huyo wa zamani wa Misri itandelea tena tarehe 15, baada ya jaji kuhairisha kesi kwa siku ya leo.
1 comment:
Siku zinakaribia za Ukombozi wa kweli Africa dhidi ya mafisadi..Fundisha kwa viongozi wetu kuwa Mwisho wa Ufisadi wao huko ukingoni..
Post a Comment