Sunday, September 4, 2011

Wanariadha wa Kenya hawana mpinzani duniani.

Muammar Gaddafi alishirikiana CIA na MI6.
Tripol, Libya - 04/09/2011.Jumuiya ya kutete haki za binadamu zimeilaumu serikali ya Uingereza na Marekani kwa kushirikiana na serikali ya Muammar Gaddafi wakati alipo kuwa madarakani.
Habari zilipo patikana zinasema "serikali ya Muammar Gaddafi ilikuwa ikishirikiana na makachelo wa CIA na MI6 na hata kuweza kutoa habari za wapinzani wa Gaddafi ambao walikuwa wanashukiwa ni magaidi, jambo ambalo lilifanya Walibya waliokuwa wamekimbia utawala wa Muammara Gaddafi kurudishwa nchini humo kwa mahojiano ili kuweza kujua kama ni magaidi au wanashirikiana na Al Qaeda."
Makaratasi zenye ripoti hizo yalikutwa kwenye ofisi inayo sadikiwa ilikuwa ya aliyekuwa mkuu wa usalama Moussa Koussa, ambaye kwa sasa anaishi nchini Katar baada ya kutoraka kwa kupitia Uingereza.
Muammar Gaddafi alikuwa mmoja wa viongozi walioshirikiana na Uingereza na Marekani katika kupambana na ugaidi na hasa kundi la Al Qaeda tangu vita rasmi vilipo tangazwa zidi ya ugaidi duniani baada ya mashambulizi ya 11/Sept 2001.
Angola ya kumbwa na vuguvugu la mabadiliko ya kisiasa.
Luanda, Angola -04/09/2011. Watu zaidi ya 23 wamekamatwa jijini Luanda baada ya kufanya maandamano ya kutaka rais Jose Eduardo dos Santos ajiudhulu.
Maandamano hayo yalianzia kwenye viwanja vya uhuru ili kuelekea kwenye ofisi za rais, kwa kuwa na lengo la kudai rais Jose Eduardo dos Santos aachie madarakani na watu walio kamatwa na kuwekwa kizuizini waachiwe huru.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka shirika la habari la Ureno Lusa zinasema " kuna baadhi ya watu wameumia vibaya wakiwemo waandishi wa habari, baada ya polisi na mafisa usalama kutumia nguvu katika kuzuia maandamano hayo."
Maandamano hayo yanakuja baada ya wanchi na viongozi wa upinzani nchini humo kudai ya kuwa "serikali ya Angola imekuwa haifanyi jitihada za kupambana na rushwa."
Angola inawananchi wapatao 16 milllion ambao wengi wao wanaisha chini ya dola 2 kwa siku.
Wanariadha wa Kenya hawana mpinzani duniani.
Daegu, Korea ya Kusini - 04/09/2011. Timu ya wanariadha wa Kenya wameweza tena kwa mara nyingine kuwanyanyu wananchi wa Afrika ya Mashariki na kuipatia sifa kubwa Kenya kwa kuweza kushinda medali za dhahabu kwa wingi kwenye mashindano ya riadha ya dunia nchini Korea.
Wanariadha hao wa Kenya wameweza kunyakua medali saba, na kukamlisha idadi ya medali kumi na sita katika mashindando hayo ambayo yanaisha wiki hii.
Vivian Cheruiyot ambaye ni mmoja ya washindi wa medali zilozo ipa sifa Kenya na Afrika ya Mashariki alisema " ushindi wetu unatokana na ushirikiano mkubwa tulionao wanariadha wa Kenya."
Wanariadha wa Kenya wamekuwa wanashinda mashindano mengi ya kimataifa na kuipatia Kenya sifa kila mwaka wanapo shiriki mashindano ya riadha popote duniani.
Dominique Strauss-Kahn arudi nyumbani akiwa huru.
Paris, Ufaransa - 04/08/2011. Aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la fedha (IFM) duniani
amewasili nchini Ufaransa baada ya kesi ya ubakaji zidi yake kufutwa hivi karibuni.
Dominique Strauss Kahn, aliwasili jijini Paris na kupokelewa na baadhi ya watu waliokuja kumlaki na hakuweza kuongea na waandishi wa habari.
Hata hivyo Strauss Kahn anakabiliwa na kesi nyingine iliyo funguliwa zidi yake na na mwandishi mmoja kwa madai "alitaka kumbaka miaka ya nyuma."
Kwa mujibu wa wafuatiliaji wa mambo ya kisiasa wa Ufaransa wanasema "kesi hizi zimemwalibia kwa kiasi kikubwa Dominique Strauss Kahn katika kampeni yake ya kutaka gombea urais nchini Ufaransa na itabidi atumie busara ili kuweza kurudisha matumaini yake ya kutaka ugombea urais."
Uchaguzi wa urais nchini Ufaransa unatarajiwa kufanyika hapo mwakani.
Muuguzi akanusha uvumi kuhusu Muammar Muammar Gaddafi.
Mogolnoye
,Ukraine -04/09/11. Mmoja wa wauguzi wa Muammara Gaddafi amekanusha madai yaliyokuwa yameenea ya kuwa kiongozi huyo Libya alikuwa na uhuusiano wa kimapenzi na baadhi ya wauguzi na walinzi wake wa kike.
Oksana Balinskaya muuguzi aliyekuwa wa Muammar Gaddafi alisema " nashangaa kusikia uvumi huo, kwani hakuna hata siku moja kati yetu alikuwa anamtibu (Dady) Muammar Gaddafi peke yake, muda wote tulikuwa tumezungukwa na watu, kama si walinzi basi watu wa falimia yake."
"Tulikuwa tuna mwita dady, kwani alivyo kuwa na ukarimu, muda wote alituuliza kama tuna shida au tunataka kitu tuseme, hivyo siwezi kusema vibaya juu yake, bila yeye nisingeweza kua hapa nilipo kimaisha nitasikitika kama akiuwawa au kukamatwa."
Oksana Balinskaya ni mmoja ya wauguzi ambao walikuwa nchini Libya ili kufanya kazi ya uuguzi wakati wa utawala wa Muammar Gaddafi ambaye ameng'olewa madarakani hivi karibinu.

Friday, September 2, 2011

Umoja wa Ulaya kuibana zaidi serikali ya Syria.

Polisi wazuia maandamano ya kimageuzi nchini Uganda.

Kampala, Uganda-02/09/2011. Serikali ya Uganda imepiga marufuko maandamano yaliyo kuwa yamepangwa ili kuungamkono mageuzi ya kisiasa yanayo endelea katika bara la Waarabu.
Uamuzi huo wa serikali umekuja baada ya habari kupatikana ya kuwa "uenda maandamano hayo yakaleta chuki kati ya jamii na kuwa mwazo wa mvurugo wa amani ndani ya nchi."
Hata hivyo msemaji wa polisi Vicent Sekate alisema " maandamano hayo yamezuiliwa kutokana na kukusa sehemu ya kuyafanyia."
Hivi karibuni rais Yoweri Museni alisema " mgeuzi yanayo tokea Kaskazini mwa Afrika yanaweza leta athari kubwa kwa bara la Afrika na kusababisha mvutano wa madaraka na kijeshi."
Serikali ya Uganda imekuwa na wakati mgumu kisiasa kutokana na joto lililomo nchini humo la kutaka serikali ya rais Yoweri Museni kufanya mabadiliko ya kiuchumi.
Umoja wa Ulaya kuibana zaidi serikali ya Syria.
Brussels, Ubeligiji -02/09/2011. Umoja wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya zimeamua kwa pamoja kuiwekea vikwazo serikali ya Syria kutokana na kukiuka haki za binadamu.
Uamuzi huo umekubalika na viongozi wa jumuia ya Ulaya ili kuibana serikali ya Syria chini ya rais Bashar al-Assad ambayop inapambana na wapinzani wanaotaka mageuzi ya kisiasa nchi humo.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alisema " tunatakiwa kuiwekea vikwazo serikali ya Syria kwani vitendo vinavyo fanywa na serikali hiyo havikubaliki."
Vikwazo hivyo ambavyo ni kuzuia ununuzi na uuzwaji wa mafuta ya Syria na kuongeza vikwazo vya usafiri kwa wale wote wanaohusika katika serikalia ya rais Assad vimesha tayarishwa na vinasubiri kujadiliwa wakati wa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa nchi hizo na baadaye kupitishwa.
Machafuko nchini Syria yamezidi kuongezeka, kufuatia mageuzi ya kisiasa yaliyo likumba bara la Waarabu hivi karibu.
Uturuki yapunguza uhusiano na Izrael.
Ankara, Uturuki -02/09/2011. Serikali ya Uturuki imeamua kupunguza uhusiano uliopo kati yake na serikali ya Izrael.
Waziri mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu aliyaongea hayo muda mfupi kabla ya katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon kukabidhiwa ripoti kuhusu tukio la jeshi la Izrael na wanaharakati waliokuwa wanelekea maeneo ya Gaza ili kupeleka misaada ya kiutu.
Serikali ya Uturuki imekuwa ikiitaka serikali ya Izrael kuomba msamaha baada ya raia wa Uturuki kuuwawa katika boti zilizokuwa zunaelekea Gaza hapo siku za nyuma.
Pia Uturuki imefunga ofisi zake za kibalozi nchini Izrael na kumtaka balozi wa Izrael nchini humo aondoke mara moja na kusimamisha ushirikiano wa kijeshi uliopo kati ya nchi hizi mbili.
Mvutano kati ya serikali ya Uturuki na Izrael ulizidi kuwa wa wasiwasi baada ya jeshi la Izraeli kufanya mashambulizi kwenye maeno ya Gaza miaka miwili iliyo pita na watu wengi kupoteza maisha na malinyingi kuharibiwa.

Thursday, September 1, 2011

Kenya hawatakuwa wanavaa nywele za bandia kwenye mahakama.

Kesi zidi ya machafuko ya Kenya yaanzwa kusikilizwa.
Hague, Uhollanzi -01/09/2011.Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi ya ukiukwaji wa haki za biadamu imeanza kusikiliza kesi zidi ya viongozi wanaoshutumiwa kuhusika na mauaji na machafuko yaliyo tokea nchini Kenya mwaka 2007 baada ya uchaguzi.
Washitakiwa hao ni waziri wa elimu William Ruto na ambaye alikuwa natarajiwa kugombea kiti cha urais katika uchaguzi ujao nchini Kenya.
Katika kesi hiyo " jaji wa mahakama hiyo alisema kesi hizo zidi ya washukiwa hao ipo kwa kusikilizwa na kuwapa nafasi washutumiwa kujitetea."
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa washitakiwa wanasema" hatuna wasiwasi na ukweli utaonekana kama hatna makosa."
Kesi zidi ya Ruto na wenzake inatarajiwa kuchukua muda kabla ya hukumu kutolewa.
Kenya hawatakuwa wanavaa nywele za bandia kwenye mahakama.
Nairobi, Kenya 01/09/2011. Majaji nchini Kenya hawatakuwa wanatumia maneno ya "my lord or my lady" katika mahakama nchini huma, baada ya madiliko kufanywa katika wizara ya sheria hivi karibuni.
Jaji mkuu Willy Mutunga alisema " kuanzia sasa majaji watakuwa wanatumia maneno ya Muheshimiwa or your honour na hii ndi itakuwa lugha ya mawasiliano kati ya wana sheria na mahakama na hawataruhusiwa kuvaa nywele nyeupe za bandia kichwani na vilevile kutakuwa na vazi rasmi la kuvaa wakati wa kuendesha kesi kotini."
Uamuzi huo umekuja baada ya majaji na wanasheria kutaka mabadiliko ya kisheria na mazingira ya koti yabadilishwe.
Ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku kutishia afya za watu tena.
Geneva, Uswisi - 01/09/2011. Shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia maswala ya kilomo na chakula (FAO) limeonya kuenea kwa ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku.
Habari zinasema "ugonjwa wa mafua ya ndege na kuku (H5N1 unaelekea kusambaa nchini China na Vietnam na huenda ukafika Kambodia na nchi zilizopo kwenye ukanda wa Peninsula.
Ugojwa wa mafua ya kuku na ndege ni ugonjwa ambao una madhara katika jamii na umesha poteza maisha ya watu karibu kila sehemu duniani.
Sarkozy na Cameron wasimia mkutano wa Libya nchini Ufaransa.
Paris. Ufaransa - 01/09/2011. Mataifa sitini yanakutana nchini Ufaransa ili kujadili ujenzi na mipango ya kuijenga upya nchi ya Libya ambayo uchumi wake umeharibika kutokana na vita katika harakati za kung'oa madarakani Muammar Gaddafi.
Mkutano huo ambao umeitishwa na rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron, unatarajiwa kuitambua rasmi serikali ya mpito na kujadili njia ya kuwasaidia wa Libya ili kuinua uchumi wao.
Mustafa Abdel Jalil mwenyekiti wa serikali ya mpito alisema " tutaweka wazi muswada wetu wa kuunda katiba mpya na kujiandaa na uchaguzi baada ya miezi 18."
Habari kutoka kwenye mkutano huo zinasema " mkutano huo utakuwa wa hali ya juu, kwani nchi ambazo zilisaidia katika harakati za kumng'oa Muammar Gaddafi madarakani zitakuwa na wakati mgumu katika kujaribu kuweka masrahi yao mbele, hasa baada ya serikali ya mpito kusema zile nchi zilizo saidia katika mapinduzi zitapata malipo bora."
Mkutano huo wa Paris unafanyika wakati Muammar Gaddafi ametangaza tene kupitia TV na radio za nchini Syria ya kuwa atapambana hadi kufa na kuwataka wale wanao muunga mkono kupigana hadi mwisho.

Wednesday, August 31, 2011

Mahakama kuu yapingana na serikali juu ya wakimbizi nchini Australia.

Waumini wa dini ya Kislaam washerekea kumaliza mwezi wa Ramadhani.
Makka, Saud Arabia 31/08/2011. Waumini wa dini ya Kislaam duniani wamesherekea sikukuu ya Iddi baada ya kumaliza mwezi wa Ramadhani.
Sikukuu ya Iddi huwa inasherekewa na waumini wa dini ya Kislaam kwa kumaliza mwezi Ramadhani baada kufunga -kwa kujizuia kula kwa kipindi chote cha mwezi mzima ikiwa njia ya kuomba toba.
Mwezi huu wa Ramadhani, waumini wa dini ya Kislaam, huwa wanaamini ya kuwa nikipindi cha kufanya mema na kutafakali yale yote waliyo yafanya na pia kumwomba "Mungu awasamehe zambi kwa huruma yake." Pia kuangali ni kwa kiasi gani watajitahidi kufanya mazuri zaidi katika maisha yanayo fuata.
Mahakama kuu yapingana na serikali juu ya wakimbizi nchini Australia.
Sedney, Australia - 31/08/2011. Mahakama kuu nchini Australia imezuia amri ya serikali ya kutaka kubadilishana wakimbizi waliopo nchini humo na wakimbizi waliopo nchini Malaysia.
Uamuzi huo wa mahakama umekuja baada ya serikali ya Australia na Malaysia kukubaliana kubadilishana wakimbizi mapema mwezi May mwaka huu.
Makubaliano hayo yalikuja wakati mawaziri wakuu wa nchi hizo walipokutana na kujadili mbinu za kuzuia biashara ya kusafirisha watu kati ya nchi hizo.
Katika kutoa hukumu hiyo, mahakama ilisema "Malaysia siyo nchi mwanachama katika makubaliano ya maswala ya ukimbizi ya mwaka 1959 chini ya umoja wa mataifa na hivyo wakimbizi wanatakiwa wapewe haki sawa kwa kufatia sheria za kimataifa na zakitaifa."

Tuesday, August 30, 2011

Zimwi la vita vya Irak bado la mwandama Tony Blair.

Zimwi la vita vya Irak bado la mwandama Tony Blair.
London, Uingereza - 30/08/2011. Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair anakabiliwa na wakati mwingine mgumu baada ya aliyekuwa mkuu wa usalama wa MI5 kudai alimwonya kuhusu vita vya Iraq.
Blair anakabiliwa na wakati mgumu baada yaaliyekuwa mkuu wa usalama wa MI5 Baroness Manningham-Buller kusema ya kuwa alimtahadhalisha na kumtaka ashughulikie kwa ukaribu zaidi vita zidi ya kundi la Al Qaeda.
Manningham-Buller aliongea kwa kusema "nilimwonya nakumweleza ya kuwa kitendo cha kuimshambulia serikali ya Sadam Hussein kijeshi, kutafanya hali ya usalama wa nchi kuwa na matatizo na hasa kutaonekana kama kushambulia dini ya Kiislaam, na ingefaa tuelekeze nguvu katika kupambana na kundi la Al Qaeda ambalo lina maficho nchini Afghaistan, kwani Irak haikuwa tishio katika usalama wa Uingereza."
Barroness Manningam-Buller ambaye amestaafu kazi mwaka 2007, aliongezea kwa kusema "vita vya Irak vimevuga mkakati wa kupambana na kundi la AlQaeda."
Kufuatia kauli hiyo ya mkuu wa usalama wa MI5, kumefanya baadhi ya wanasiasa kuanza kuuliza maswali mengi kwanini Uingereza iliishambulia Irak.
Mke wa Gaddafi na watoto wake wakimbilia Algeria na wapinzani watoa onyo la mwisho.
Algiers, Algeria -30/08/2011. Mke wa pili wa aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi amekimbilia nchini Algeria pamoja na watoto wake.
Habari kutoka ofisi ya wizara ya mambo ya nchi za nje zimesema " Safia Gaddafi aliwasi saa 08:45 na watoto wake Aisha, Hannibal na Mohammed na tumewapokea kiutu jambo ambalo kila mtu anahitaji kupewa."
Mahmud Shammam msemaji wa serikali ya mpito alisema " kitendo cha Algeria kuipokea famila ya Gaddafi ni kinyume na matwakwa ya Walibya na tutaomba warudishe nchini Libya waje wajibu mashitaka ya kutumia mali ya umma vibaya."
Serikali ya Algeria ilikuwa na uhusuano mzuri na serikali ya Muammar Gaddafi kwa kipindi kilefu na mpaka sasa imekataa kuitambua serikali ya mpito ya Libya.
Wakati huo jeshi la serikali ya mpito limetoa onyo la mwisho kwa wanajeshi ambao wanamuunga mkono Muammar Gaddafi kusalimu amri au kuwatayari kwa mapambano ikifika siku ya Jumamosi.
Onyo ilo limekuja wakati jeshi la wapinzani likiwa limezingira mji Sitre ambao unasadikiwa kuwa kuna nguvu nyingi za kijeshi na nimji alio zaliwa Muammar Gaddafi.
Mahakama ya haki za binadamu yakataa maombi ya Kenya.
Nairobi, Kenya -30/08/2011.Rufaa ya serikali ya Kenya kwenye mahakama ya kutetea haki za binadamu imekataliwa na mahakama iliyopo nchini Uhollanzi.
Rufaa hiyo ambayo ilikuwa imeitaka mahakama ya Hague kusimamisha kesi zidi ya washitakiwa sita akiwemo makamo wa waziri mkuu, mawaziri , mmoja wa mkuu wa polisi na viongozi wengine waliohusika katika kuchochea machafuko baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa mwaka 2007.
Kesi hiyo ina tarajiwa kuanza siku ya Alhamisi wiki hii, ambapo washitakiwa hao wanatakiwa kujibu mashitaka zidi yao kwa kuhusika na machafuko yaliyo sabaisha mauaji na mali nyingi kuteketea.
Kesi hiyo ilifunguliwa baada ya mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo Luis Moreno -Ocampo kumaliza uchunguzi wake aliyo ufanya nchini Kenya baada ya machafuko kutokea.
Serikali ya Zimbabwe yamfukuza balozi wa Libya.
Harare,
Zimbabwe - 30/08/2011. Serikali ya Zimbabwe imemfukuza balozi wa serikali ya mpito ya Libya baada ya kutamka ya kuwa anaunga mkono serikali ya mpito iliyo mpindua Muammar Gaddafi.
Taher Elmagrahi, alitangaza kuiunga mkono serikali ya mpito na kujiunga nayo baada ya serikali ya Muammar Gaddafi kung'olewa hivi karibuni na jeshi la wapinzani.
Simbarashe Mumbengegwi waziri wa mambo ya nchi za nje wa Zimbabwe alisema " Elmagrahi na wafanyakazi wote wa ubalozi wanatakiwa kuondoka nchini katika kipindi cha masaa 72."
Hata hivyo Taher Elmagrahi aliseme " mimi siyo mtu wa Muammar Gaddafi nipo kwa aajili ya Walibya na nawakilisha Walibya."
Serikali ya Zimbabwe na Libya zimekuwa na uhusiano wa karibu sana, hasa kati ya Muammar Gaddafi na rais Robert Mugabe.

Monday, August 29, 2011

Mbu wa malaria waelekea kupungua nchini Tanzania.

Serikali ya Marekani kukabiliana na maafa ya Irine.
Washington, Marekani - 29/08/2011. Kimbunga na mafuriko ambacho kimetokea nchini Marekani kimesababisha uaribifu mkubwa na kupoteza maisha ya watu kwa mujibu serikali.
Mafuriko hayo na kimbunga ambacho kilianza wiki iliyopita yamesababisha nyumba na barabara kubomoka na kufanya hali ya maisha na mawasiliano kuwa ngumu.
Craig Fugate mkurugenzi mkuu wa maswala ya maafa alisema" serikali ina kibarua kigumu na itajitahidi kuwasaidia wale wote waliokumbwa na kumbunga Irine na kiasi cha mamillioni ya dola zinahitajika haraka sana ili kuanza kutoa huduma."
Kimbunga na mafuriko yaliyo sababishwa na Irine kimefuatia kimbunga Katalina kilicho sababisha maafama makubwa miaka michache iliyopita nchini Marekani.
Mbu wa malaria waelekea kupungua nchini Tanzania.
Dar es Salaam, Tanzania - 29/08/2011. Watafiti wa malaria nchini Tanzania wamedai yakuwa mbu ambao wanasababisha ugonjwa wa malaria wanaelekea kupungua.
Wanasayansi wa Tanzania na Denmarki wamegundua upunguaji wa mbu hao baada ya kufatilia idadi ya mbu ambao walikuwa wanapatikana na viini vya ugonjwa huo.
Profesa Dan Meyrowisch, alisema " upunguaji wa mbu hao ni kitu ambacho kinatakiwa kufanyiwa uchunguzi zaidi, ingawa inaweza sababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa na ukame."
Mpango wa kupambana na malaria umekuwa ikipewa kipao mbele ili kutokomeza malaria katika bara la Afrika ugonjwa ambao umekuwa unasababisha vifo vingi hasa kwa watoto wadogo.
Mshukiwa wa ulipuaji wa ndege ya Pan am jet anahali mbaya kuliko ilivyo zaniwa.
Tripol, Libya 29/08/2011. Mshukiwa ambaye inasadikiwa alihusika katika ajali ya ndege Pan Am Jet amekuwa na hali mbaya kiafya kuliko ilivyozaniwa na viongozi na wanasiasa wa Uingereza na Marekani.
Mohmed al Megrahi, ambaye aliachiwa huru mwaka 2009 na serikali ya Scotland na kurudi nchini mwake Libya baada ya kujilikana ya kuwa ana ugonjwa wa saratani- kansa ambayo itamfanya kutokuishi kwa muda mrefu.
Kuruhusiwa kwa Al Mergahi kumeleta mvutano kati ya wanasiasa na viongozi wa Uingereza na Marekani kwsa wengine kudai yakuwa arudishwe nchini Scotland kuendelea na kifungo.
Khaked al Megrahi, mtoto wa Mohmed Megrahi amesema " baba yangu ni mgojwa sana nahakuna mganga wala muhudumu ambaye tunawasiliana naye na hakuna msaada wowote tunapata, baba anatumia oksijeni na dawa zake zimekwisha hivyo tupo naye na hatujui nini la kufanya."
Waziri wa sheria wa serikali ya mpito Mohamed al Alagi alisema, hakuna Mlibya yoyote atakaye pelekwa nchi za magharibi ili kujibu mashitaka, hivyo Mohmed al Megrahi atapelekwa kokote."
Nayo serikali ya Scotland imesema " alifanya jambo la kiutu na Mohmed al Magrahi hatarudishwa nchini, na ushahidi umeonyesha yakuwa tulivyo amua kumuachia kwani hali yake sasa siyo nzuri."
Mashariki ya Uganda yakumbwa na maporomoko.
Kampala
,Uganda -29/08/2011. Mapoloka makubwa yameokea mashariki mwa Uganda na kusabaisha vifo vya watu na uharibifu mkubwa.
Msemaji wa shirika la msalaba mwekundu Catherin Ntabade alisema " mvua kubwa iliyonyesha ndiyo iliyo sababisha maporokomo hayo na hadi sasa watu wapatao 23 wamepoteza maisha na watu wengine hawajulikani wapo wapi."
Serikali ya Uganda imepeleka kikosi cha waokoaji na misaada mingine ili kukabiliana na tukio hilo.
Maporooko kama haya yalitokea mwaka jana kwenye eneo karibu na mlima Elgon kwenye mpaka wa Kenya na Uganda na kuleta maafa makubwa kwa jamii na mazingira.

Sunday, August 28, 2011

Mapadri wazidi kujitoa katika Kanisa Katholiki nchini Kenya ili kuoa.

Al Qaeda namba mbili auwawa.
Islambad, Pakistan - 28/02/2011.Kiongozi wapili kimadaraka katika kundi la Al Qaeda ameuwawa nchini Pakistani.
Atiya Abdul Rahman raia wa Libya ambaye inaaminika alikuwa muhimu katika kupanga mbinu zote za mashambulizi la kundi la Al Qaeda na alikuwa anawasiliana moja kwa moja Osama Bin Laden ambaye aliuwawa miezi michache iliyopita.
Kifo cha Atiya Abdul Rahman, kinasadikiwa ni pigo kubwa kwa kundi hilo, kwani ndiye mtu ambaye alikuwa "anaweza kumsaidia kiongozi wa sasa wa Al Qaeda Ayman al Zawahiri katika kuimarisha kundi hilo."
Kifo chake kimetokea baada ya ndege ya kijeshi inayo endeshwa na ongozwa na mtandao kushambulia eneo alilo kuwa amejificha.
Kundi la Al Qaeda lina ongozwa na Ayman al Zawahiri,baada ya kifo cha kiongozi wa kundi hilo Osama bin Laden.
Mapadri wazidi kujitoa katika Kanisa Katholiki nchini Kenya ili kuoa.
Nairobi, Kenya - 28/08/2011. Zaidi ya mapadri 40 wameamu kujitoa katika kanisa Katoliki na kujiunga na Kanisa la Ekumenikal Katholik ili waweza kuoa na kuwa nafamilia kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita.
Askofu wa Kanisa la Ekumenikal Katholik, Geoffrey Shiundu, ambaye alijitoa katika kanisa mama la Katholik baada ya kuamua kuoa, alisema "kanisa la Ekumenikal linazidi kukua na mapadri wanadizi kujiunga nalo."
"Tutaweza kushirikiana na kanisa mama la Katholik kama Papa Benedikt XVI atakubali kubadili muundo wa kanisa kwa kuweka huru, ikiwa padri anataka kuoa aoe na kama hataki basi abaki bila kuoa." Alisisitiza.
Askofu Shiundu aliyasema hayo wakati wa sherehe ya kumweka wakfu mmoja wa mapadri kwenye mji wa Kitale.
Libya yarudishiwa uanachama na jumuiya ya nchi za Kiarabu.
Kairo
,Misri - 28/07/2011. Shirikisho la nchi za jumuiya ya Kiarabu remeirudishia uanachama wake Libya baada yakuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi.
Msemaji wa jumuiya hiyo Nabil Elarab alisema " bendela mpya ya serikali ya mmpito itawekwa na ile ya serikali ya Muammar Gaddafi ambayo ilikuwa na rangi ya kijani itatolewa."
Libya ilitolewa katika jumuiya hiyo baada ya serikali ya Muammar Gaddafi kuanza kupambana na wapinzani waliokuwa wanaipinga serikali yake mapema mwezi wa pili mwaka huu.

Friday, August 26, 2011

Mlipuko wa bomu watokea katika majengo ya ofisi za umoja wa mataifa.

Umoja wa Afrika wachanga pesa ili kusaidia maeneo yaliyo kumbwa na ukame.

Adis Abeba, Ethiopia - 26/08/2011. Viongozi na marais wa Umoja wa Afrika wamekutana jijini Adis Abeba na kubaliana na kutoa mchango wa fedha kiasi cha £215milioni ili kusaidia maeneo ambayo yamekumbwa na ukame katika bara la Afrika.
Akiongea katika mkutano huo wa kuchangisha fedha, katibu msaidizi wa umoja wa mataifa Asha Rose Migiro alisema " bado tunaitajika kutoa misaada kwa wananchi wengi ambao wamekumbwa na ukame ili kuzuia janga la vifo na kupoteza kizazi kijacho cha bara la Afrika, na uwezo tunao wa kuzuia hali hii isiendelee kama tukishirikiana."
Katika mkutano huo pia benki ya Afrika iliahidi kuongeza juhudi zake za kuimarisha uchumi kwa kuwekeza zaidi katika miradi itakayo leta maendeleo kwa wananchi.
Kufanyika kwa mkutano huo wakuchangisha pesa, umekuja baada ya mashirika ya kimataifa kudai ya kuwa "umoja wa Afrika hauja lipa kipao mbele swala la kame lililo likumba bara hilo."
Serikali ya Uganda yatupilia mbali hukumu ya vifo kwa mashoga.
Kampala, Uganda - 26/08/2011. Serikali nchini Uganda limetupilia mbali muswada wa kutaka mashoga na kwa wale wote ambao wanapenda kufanya mapenzi kijinsia moja kupewa adhabu ya kifo.
Waziri wa serikali za mitaa, Adolf Mwesige alisema " serikali inapinga kitendo hicho, na kwa sasa kunasheria za kutosha za kushughulikia swala hilo."
Mswada huo wa kuwapa adhabu kali mashoga na watu wenyekupenda kufanya mapenzi kijinsia moja ulipendekezwa na mwaka 2009 na mbuge David Bahati, jambo ambalo lilifanya dunia nzima kutupia mcho yake nchini Uganda ili kutetea haki za watu hao.
Hata hivyo asilimia 90 ya wananchi wa Uganda wanapinga tabia za mashoga.
Naye mmoja wa watu ambao wanaunga mkoo kutupiliwa mbali kwa muswada huo alisema " huu ni ushindi kwa aliye kuwa mtetezi wetu David Katto, ambaye aliuwawa katika harakati za kutete haki sawa kwa kila Mganda."
Hata hivyo habari kutoka bunge la Uganda zinasema, "rais Yoweli Museveni, aliwaambia wabunge yakuwa wapunguze munkali na swala la mashoga, kwani kuna mambo mengi ambayo yanatakiwa kufanywa katika kuinua maisha ya wananchi.
Mlipuko wa bomu watokea katika majengo ya ofisi za umoja wa mataifa.
Abuja, Nigeria -26/08/2011. Milipuko ya mabomu imetokea katika jengo ambalo kuna ofisi za umoja wa mataifa na kuleta maafa makubwa.
Kwa mujibu wa mashaidi walio ona tukikio hilo walisema" mlipuko huo ulitokea baada ya gari moja kuvuka kizuizi cha kuingilia katika jengo hilo."
Naye katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban ki - Moon amelaani kitendo cha kulipuliwa ofisi za umoja huo na muuaji wa kujitolea muanga kwa kusema " ni kitendo hambacho hakionyeshi nia njema kwa wale wote ambao wanajitolea kufanya kazi ya kusaidia jumuiya za kimataifa."
Kufuatia mlipuko huo katibu msaidizi Rose Migiro atawasili nchini Nigeria ili kuongea na viongozi serikali na kupata habari kamili kwa ajili ya kuziwakilisha kwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa.
Naye msemaji wa polisi Yemi Ajavi alisema "watu kadhaa wameumia vibaya na wengine kupoteza maisha na inaonekana kama ni mauaji ya kujitolea muhanga na mpaka sasa bado tupo katika harakati za uokoaji kwani kuna baadhi ya watu bado wamekwama ndani ya jengo hilo."
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amelaani kitendo hicho na kusema " serikali itafanya kila njia kuwakamata wale wote walio husika katika mashambulizi hayo."
Kundi linalo julikana kama Bokaharamu limedai kuhusika na ulipuaji wa ofisi hizo za umoja wa mataifa, na kusema " uhu ni mwanzo wa kujibu mashambulizi baada ya serikali kutuma jeshi lake katika eneo la Kaskazini la Borno na kuna watu 100 ambao wapo tayari kujitolea muanga." Alisema msemaji wa kundi hilo Abu Darda.
Mlipuko huu wa bomu katika ofisi za umoja wa mataifa ni moja ya milipuko ya mabomu ambayo imekuwa ikitokea nchini Nigeria ambapo hivi karibuni bomu lililipuka katika ofisi za makao makuu ya jeshi la polisi jijini Abuja.

Thursday, August 25, 2011

Zawadi nono kutolewa kwa atakaye toa habari alipo Gaddafi akiwa mzima au amekufa.

Jean-Pierre Bemba kugombea urais wa Kongo DR.
Kinshasa, Kongo DR - 25/08/2011. Kiongozi wa chama cha upinzani nchini Kongo, naambaye yupo chini ya mahakama ya kimataifa ya kuzuia hualifu amehaidi kugombea kiti cha urais katika uchaguzi unao tarajiwa kufanyika mwisho wa mwaka 2011.
Jean Pierre Bemba ambaye ni kiongozi wa chama- MLC, Movement Liberation of Congo amesema hayo kupitia mwanasheria wake Aime Kilolo ya kuwa "atagombani kiti cha urais ijapokuwa yupo na kesi."
Memba ambaye alikamatwa 2008 nchini Uberigiji na kufunguliwa kesi ya kukiuka haki za binadamu kwenye mahakama ya kutetea haki za binadamu iliyopo Hague nchini Uhollanzi wakati wa jeshi lake lilipo kuwa linapambana na jeshi la serikali kati ya mwaka 2002 na 2003
Habari zilizo patikana zinamsema akiwa kizuizini Jean Pierre Bemba ameweza kutana na wakongo wengi wakiwemo viongozi wa upinzani Etiene Tshisekedi, Vital Kamerhe na Leon Kengowa Dondo.
Zawadi nono kutolewa kwa atakaye toa habari alipo Gaddafi akiwa mzima au amekufa.
Benghazi,
Libya -25/08/2011. Serikali ya mpito ambayo inapambana katika kuing'oa madarakani serikali ya Libya imetangaza kutoa zawadi ya fedha kwa mtu yoyote atakaye toa habari wapi yupo kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi ili akamtwe akiwa mzima au amekufa.
Guma el Gamaty ambaye ni mmoja wa viongozi wa serikali ya mpito, alisema " hii ni nafasi ya dhahabu ya $ 1.7million zitatolewa ikiwa mtu yoyote atatoa habari za kupatikana kwa Muammar Gaddafi"
Zawadi hii imetolewa na wafanya biashara kwa kusaidia na serikali ya mpito ambayo wapiganaji wake wanapigana na serikali ya Muammar Gaddafi.
Nayo serikali ya Itali imekubali kuachilia pesa za zilizo kuwa za serikali ya Muammar gaddafi ili kusaidia serikali ya mpito.
Hadi sasa Muammar Gaddafi na familia yake hawajulikani wapo wapi, baada ya kundi la upinzani kuingia katika jiji la Tripoli hivi karibuni.

Wednesday, August 24, 2011

Muammar Gaddafi ahaidi kufa au kupata ushindi.

Samuel Eto'o avunja rekodi ya dunia kuwa mchezi wa mpira wa miguu kwa kulipwa pesa nyingi.
Dagestan, Urussi 24/08/2011. Mchezaji maharufu wa mpira waamiguu wa timu ya taifa ya Kameroon na Inter Milan Samuel Eto'o amevunja rekodi ya duia kwa kuwa mchezaji atakeye lipwa pesa nyingi baada ya kusaini mkataba na timu ya Anzhi Makhachkala iliyopo katika jimbo la Dagestan.
Samuel Eto'o , ambaye ameshinda kombe la ligi ya vilabu bingwa vya ulaya wakati akichezea timu Barcelona na Inter Milan, anatarajiwa kupokea kiasi cha 28.8million kwa muhula baada ya kusaini mkataba wa miaka mitatu kuchezea timu hiyo.
Eto'o atakuwa anapokea kiasi cha 350,000 kwa wiki kuliko wacheza wengine maarufu dunia ambao ni Wesley Snijder anapokea 250,000 kwa wiki, Christian Ronaldo 210,000 na mchezaji bora wa dunia Lionel Messi 180,000.
Akiongea baada ya kusaini mkataba Eto'o alisema " napenda kuwashukuru wapenzi na viongozi wa Inter Milan kwa kuonyesha mapenzi na ushirikiano kwa kipindi chote nilipo kuwa mchezaji na mkazi wa jiji la Milani.
Mapambano ya kikabila kutishia amani Kusini mwa Sudani.
Juba, Sudani ya Kusini -24/08/2011.Shirika la umoja wa mataifa -UNMISS - linaloshirikiana na serikali ya Sudani ya Kusini-,limeonya ya kuwa mauaji ya kikabila bado yanaendelea katika jimbo la Jongle.
Katika ripoti iliyo tolewa na shirika hili zinasema " watu wa jamii ya Murle na Lou Nuer wamekuwa wakipigana katika harakati za kutaka kila jamii iwe na mifugo mingi jambo ambalo ilinatishia amani katika eneo hilo"
Ripoti hiyo imeongezea ya kuwa katika maeneo hayo "bado kuna uhaba wa mahitaji muhimu ya kijamii."
Hata hivyo habari kutoka serikali ya Sudani ya Kusini zinasema " eneo hilo limeanza kupewa kipao mbele na itachukua muda kukamilisha miradi yote kutokana na mazingira ya kijiografia."
Sudani ya Kusini iliundwa baada ya kura ya maoni ya kutaka eneo hilo lijitenge kutoka serikali ya Kartoum, na kujitangazia utawala wake hivi karibuni.
Muammar Gaddafi ahaidi kufa au kupata ushindi.
Libya, Tripol -24/08/2011.Kiongozi wa Libya amelihutubia taifa kwa kutumia redio, huku mahali alipo ajulikani baada ya jeshi la wapinzani kuchukua makazi ya kiongozi huyo ya Bab al Aziziya na karibu maeneo ya jiji la Tripol.
Kanali Muammar Gaddafi, alisema "tunapigana vita zidi ya wasaliti wa Libya na katika mapambano haya kuna mambo mawili kufa au ushindi, na kitendo cha mimi kutoka hapo Bab al Aziziya ni mbinu za kujipanga tayari kwa mashambulizi, kwani tulijua ya kuwa NATO walikuwa wanataka kushambulia eneo hilo."
Naye msemaji wa serikali ya Libya, Mussa Ibrahim, akisisitiza kwa kupitia TV kutoka eno lisilo julikana alisema " Libya itakuwa na mlipuko wa volkano, majivu na moto na tunauwezo wa kupigana kwa muda mrefu."
Hata hivyo viongozi wa serikali ya mpito wamedai yakuwa "Muammar Gaddafi ameshaangushwa na tunampango wa kuamishia ofisi zote jijini Tripoli muda si mrefu na tunaendelea kumsaka hadi tu mkamate na ndipo Walibya watakuwa huru."
Hadi kufikia sasa Muammar Gaddafi na familia yake awajulikani wapo wapi jambo ambalo bado lina leta mashaka kwa serikali ya mpito.
Makampuni ya mafuta kusuguana vichwa baada ya kuanguka kwa Gaddafi
Paris
,Ufaransa 24/08/2011.Viongozi na wafanya biashara wa maampuni ya mafuta wamekuwa wakivutana nyuma ya ukuta na kusuguana vichwa, katika majadiliano ya keweza kukubaliana na serikali ya mpito ya Libya ni kwa jinsi gani uchimbaji na upatikanaji wa mafuta utakavyo kuwa.
Hali hii inakuja baada ya serikali ya mpito kutangaza ya kuwa itaaangalia mikataba yote iliyo wekwa na serikali ya Muammar Gaddafi.
Habari kutoka ndani ya serikali hiyo ya mpito zinasema, " makampuni yote ambayo yanatoka kwenye serikali ambazo hazikushiriki katika kuunga mkono kung'olewa kwa Gaddafi huenda mikaaba yao ikafutwa."
Kufuatia habari hizi baadhi ya serikali zilizo tiliana mikataba na serikali ya Gaddafi "zimeshaanza mikakati ya kutaka kulinda mikataba hiyo kwa kila hali."
Libya ni moja ya nchi yenye utajiri mkubwa wa mafuta na tangu kuanza kwa vita nchin humo bei katika soko la mafuta imekuwa ikiyumba.

Tuesday, August 23, 2011

Kesi zidi ya Dominik-Strauss Kahn yafutwa na aachiwa huru.

Kesi zidi ya Dominik-Strauss Kahn yafutwa na aachiwa huru.
New York,
Marekani - 23/08/2011. Jaji wa mahakama amefuta kesi zidi ya aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la fadhe la kimataifa baada ya kesi hiyo kutokuwa na ushaidi wa kutosha.
Jaji Michel Obus aliamua kufuta kesi hiyo baada ya mwanasheria kwa upande wa mashitaka kudai ya kuwa "kesi zidi ya Dominik Strauss-Kahn haina ushaidi wa kutosha kwa kuzingatia ukweli wa bi Diallo ambao ameusema alipo wasili nchini Marekani."
Mwanasheria Kenneth Thompson ambaye anamtete mshitaki alisema" mwanasheria wa serikali ameamua kutokubaliana na haki ya mwanamke asiyekuwa na makosa kuweza kupata haki yake kutokana mambo yaliyomtokea."
Baada ya uamuzi wa mahakama kufuta kesi, familia ya Strauss-Kahn ilisema " kipindi chote cha kesi hii familia yetu ilikuwa aina furaha na kuanzia sasa tunaweza kuanza upya maisha ya kujenga familia yetu ."
Kufuatia uamuzi wa mahaka kufuta kesi, Dominik Strauss-Kahn yupo huru na anaweza kusafiri kurudi nchini kwake Ufaransa.
Dominik Strauss-Kahn alifunguliwa mashitaka baada mfanyakazi katika hotel aliyo kuwa amefikia kufungua kesi ya ubakwaji zidi yake.

Vita vya LIbya vyaingia sura mpya na Saif al Islaam yupo huru.

Afrika ya Kusini na Burundi zasahini mikataba ya kiuchumi.
Bujumbura, Burundi -23/08/2011. Serikali za Afrika ya Kusini na Burundi zimetiliana sahii mikataba ya kiuchumi kati ya nchi hizo ili kuimarisha maendeleo na kukuza ukaribu zaidi
Mikataba hiyo ilisainiwa wakati rais wa Afrika ya Kusini, Jakob Zuma alipo fanya ziara ya kiserikali nchini Burundi, ili kudumisha ushirikiano uliopo kati ya nchi hizo mbili, na kwa kuzingatia rais Jacob Zuma alikuwa mmoja wa wasuruhishi katika jitihada za kuleta amani nchini Burundi.
Katika mikataba hiyo nchini hizo zitashirikiana katika sekta za kilimo,usafiri na kifedha, ambapo kutaongezea nguvu kiuchumi hasa kwa nchi ya Burundi ambayo ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa muda mrefu hadi vilipo kwisha hivi miaka ya karibuni.
Vita vya Libya vyaingia sura mpya na Saif al Islaam yupo huru.
Tripoli
, Libya - 23/08/2011.Mtoto wa kiume wa kiongozi wa Libya ameonekana na kuongea na waandishi wa habari, masaaa machache baada ya kundi la upinzani kutangaza yakuwa wame mkamata yeye na ndugu zake.
Huku akishangiliwa na wadau na wale wanao muunga mkono baba yake, Saif al-Islaam alisema " mimi nipo na kundi la wapinzani limekwisha na utiwake wa mgongo umesha uvunja. Na baba yangu yupo salama na tutashinda zidi yawale wanaotaka mali ya Libya."
Pia alimalizia kwa kusema" kesi zidi ya mahakama ya kimataifa ya Uhollanzi hainisumbui kichwa na kwasasa kundi la upinzani limekwisha na jiji la Tripol lipo chini ya mikono yetu."
Kufuatia kuoneana kwa Saif al Islaam, viongozi wa kimataifa wamekuwa wakitoa maelezo tofauti na kusisitiza yakuwa muda si mrefu utawala wa Muammar Gaddafi utaporomoka na Libya itakuwa huru.
Saif al Islaam ambaye alizaniwa kuchukua madaraka ya baba yake, amekuwa ndiye msemaji mkuu wa serikali ya baba yake na kuhaidi yakuwa serikali ya baba yake itashinda.

Monday, August 22, 2011

Serikali ya Tanzania yaonya viongozi wanaoshiriki biashara ya madawa ya kulevya.

Serikali ya Tanzania yaonya viongozi wanaoshiriki biashara ya madawa ya kulevya.
Dar es Salaam, Tanzania - 22/08/2011. Serikali ya Tanzania imeonya yakuwa wale viongozi wa dini na serikali wanao tumia madaraka yao katika kufanya biashara ya madawa ya kuleva watakamatwa muda si mrefu.
Akiongea na waandishi wa habari, mkuu wa kitengo cha kupambana na madawa ya kulevya
Godfley Nzowa alisema "tumepata majina ya watu wanaohusika na biashara hizo na bado tunafanya kazi ya uchunguzi zaidi ili kuwakamata wahusika wate. Na kunabaadhi ya majina tuliyo nayo ni yaviongozi wa dini na serikali wanaohusika katika biashara hiyo haramu."
Akijibu shutuma hizo kiogozi wa kanisa Katoliki, Kadinal Polycarp Pengo aliomba serikali iwataje viongozi hao wa dini ili kuthibitisha ukweli huo na kujenga imani kwa wananchi.
Onyo hilo limekuja baada ya ripoti kutoka ofisi za umoja wa mataifa zinazo shughulika na kupambana na madawa ya kulevya kuelezea ya kuwa "eneo la Afrika Mashariki limekuwa nikitovu cha kupitishia madawa ya kulevya kutokea Pakistani na sehemu tofauti duniani na kuwa ndio biashara kubwa inayo fanywa na wafanya biashara wakubwa na kukuza uharifu katika nchi za maeneo haya."
Serikali ya Afrika ya Kusini kuwa mwenyeji mkutano wa hali ya hewa na mazigira.
Durban, Afrika ya Kusini - 22/08/2011.Idara inayoshughulikia haliya hewa na mabadiliko yake ya umoja wa mataifa imeaanza maandalizi ya mkutano utakao fanyika nchini Afrika ya Kusini kuanzia Desemba 4 mwaka huu.
Kwa mujibu wa habari zinasema, "mkutano huo utawakusanyisha wajumbe wapatao 20,000, viongozi na wakuuu wa nchi wapatao 100."
Mkutano huo ambao ni moja ya mikutano ya kujadili hali halisi ya mabadiliko ya hali ya hewa,utajadili mikakati ya kupambana na uharibifu wa mazingira unaofanywa duniani kote.
Jiji la Tripoli lazungukwa na milio ya risasi baada ya jeshi la wapinzani kuingia.
Tripoli, Libya 22/08/2011.Jeshi la kundi la upinzani linalo pingana na serikali ya Libya limeingia jiji Tripoli kwa mara ya kwanza na kukamata badhi ya maeneo katika jiji la Tripoli.
Msemaji kundi hilo la kijeshi Guma El- Gamati alisema " Wapiganaji wetu wanashikilia karibu sehemu zote za jiji la Tripoli na jeshi la serikali lina shikilia maeneo matatu ambayo ni hospital, kambi ya kijeshi na Rixo Hotel na baadhi ya wapiganaji wa jeshi la Libya wamekuwa katika mazungumzo ya kusalimu amri ili kujisalimisha kwa jeshi letu."
Na habari kutoka kwa kiongozi wa jeshi la upinzani zinasema " mtoto wa Muammar Gaddafi ,Saif al Islam Gaddafi amekamatwa na jeshi hilo la upinzani na sasa yupo chini ya ulinzi wao."
Hata hivyo hakuna habari kutoka serikali ya Libya juu ya kukamatwa kwa mtoto huyo wa Muammar Gaddafi, ila msemaji wa serikali Mussa Ibrahim alisema mashambulizi yalyofanywa siku ya jumapili yameua zaidi ya raia 1,00 na zaidi ya 5000 kujeruhiwa vibaya."
Kufuatia kuingia kwa kundi hilo la upinzani jijini Tripoli, milio ya risasi imekuwa ikisikika karibu kila eneo ndani ya jiji hilo.
Mapigano kati ya jeshi la kundi la wapinzani na serikali ya MuammarGaddafi yalianza mapema mwezi machi na hadi sasa yameshafikisha miezi sita.

Sunday, August 21, 2011

Serikali ya Kenya yakasirishwa na Luis Moreno Ocampo.

Serikali ya Kenya yakasirishwa na Luis Moreno Ocampo.
Nairobi, Kenya - 22/08/2011. Serikali ya Kenya imekasirishwa na kitendo cha mwanasheria mkuu wa mahakama ya makosa ya jinai iliyopo nchini Uhollanzi, kwa kuihusisha ikulu katika machafuko ya kisiasa yaliyo tokea nchini humo.
Habari kutoka ikulu zinasema, "ofisi ya rais imekasirishwa sana na Luis Moreno Ocampo kuwahusisha wafanya kazi wa karibu wa rais Mwai Kibaki katika machafuko ya kisiasa."
Hata hivyo habari kutoka ofisi ya Luis Moreno Ocampo zinasema " ripoti hiyo haikuwahusisha rais na waziri mkuu wa Kenya."
Ripoti hiyo ya Luis Moreno Ocampo imekuja baada ya uchunguzi uliyo fanywa na ofisi yake nchini Kenya, baada ya machafuko yaliyo leta hasara kwa raia na mamia kupoteza misha kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliyofanyika nchini humo mwaka 2007 .
Wamarekani wahukumiwa kwenda jela nchini Iran.
Tehran,
Iran -22/08/2011. Mahakama nchini Iran imewahukumu raia wawili wa Marekani kwenda jela kwa kosa la kuingia nchini humo kinume cha sheria na kufanya ukachelo wa niaba ya serikali ya Marekani.
Watuhumiwa hao, Josh Fattal na Shane Bauer walihukumiwa kwenda jela miaka minane kila mmoja, baada ya ya mahakama kuwakuta na hatia na kuamua kuwahukumu miaka mitano kila mmoja kwa kosa la kufanya ukachelo na miaka mitatu kila mmoja kwa kosa la kuingia nchini Iran kinyume cha sheria.
Mwanasheria anaye wawakilisha wa Marekani hao alisema " natumani wateja wangu wataachiwa kwa msamaaha wa serikali, baada ya wazazi wa watuhumiwa hao kuiomba serikali ya Iran kuwaachia kwa kuzingatia ni mwezi mtukufu wa Ramdhani, kwani hawakufanya makosa yoyote"
Josh na Shane walikamatwa 31/Julai/2009 baada ya serikali ya Iran kudai walikuwa wamevuka mpaka na kuingia nchini humo kutokea eneo la Kikurdish lililopo nchini Irak.

Friday, August 19, 2011

Rais wa zamani wa Ivory Cost afunguliwa mashitaka.

China na Marekani zakutana kujadili mabadiliko uchumi.
Beijing, China 18/08/2011. Serikali za China na Marekani zimekubaliana kuendelea kufanya biashara ingawa kuna baadhi ya vikwazo ambavyo vipo kati ya nchi mbili hizo.
Makamu wa rais wa China akimkaribisha mgeni, wake makamu wa rais wa Marekani Joe Biden,ambaye yupo ziarani nchini China, Xi Jinping alisema "Marekani ni nchi ambayo inatakiwa kuimarika kiuchumi,kwani uchumi wake ni kiungo cha duniani."
Makamu wa rais Joe Biden yupo nchini China ilikujadili maswala ya kiuchumi na biashara na serakali ya China .
Hata hivyo habari kutoka serikali ya China zinasema, makamu wa rais Xi Jinping atazungumzia swala la Marekani kutaka kuuzia Taiwani zana za kijeshi.
Rais wa zamani wa Ivory Coast afunguliwa mashitaka.
Abidjani
, Ivory Coast 12/08/2011.Rais wa zamani wa Ivory Coast amefungulia mashitaka ya kutumia mali ya umma vibaya wakati akiwa madarakani .
Laurent Gbagbo, ambaye alitolewa madarani kwa nguvu na jeshi la rais wa sasa Alassane Outtara, anakabiliwa kujibu mashitaka ya kutumia fedha na mali za serikali kabla na baada ya uchaguzi kwa manufaa ya kumsaidia kubaki madarakani.
Hata hivyo wasemaji wa kutetea haki za binadamu, hawakulizika na kesi hiyo kwa madai ni "haina uzito kulinganisha na mauaji na uharibifu uliyo tokea wakati wa vita kati ya wanajeshi wa Gbagbo na Outtara mara ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa baaada ya Laurent Gbagbo kudai yakuwa yeye ndiye alishinda uchaguzi.