Thursday, July 21, 2011

Mahakama ya Uingereza yaruhusu kesi ya rais wa Kenya kuendelea.

Mahakama ya Uingereza yaruhusu kesi ya rais wa Kenya kuendea.
London, Uingereza - 21/07/2011. Mahakam kuu nchi Uingereza imekubaliana na maombi raia wa Kenya kuishitaki serikali ya Uingereza kwa kuhusika na mauaji na mateso wakati wa kundi la Mau Mau lilipo kuwa lipinga ukoloni.
Jaji katika mahakama hiyo Richard McCombe ambaye alitoa uamizi huo alisema " Washitaki wanaweza kuendelea na kesi hii, kwani ushaidi wa kisheria upo kwa serikali ya Uingereza kujibu mashitaka haya."
Katika kesi hiyo, serikali ya Uingereza imekuwa ikijitaihidi kupinga kuendelea na kesi hiyo, kwa madai yakuwa hilo ni" jukumu la serikali ya Kenya."
Wawakilishi katika kufungua kesi hiyo Ndiku Mutwiwa Mutua, Paulo Muoko Nzili, Mbugua Wa Nyingi na Jane Muthoni Mara ambao wapo na umri kati ya miaka 70 na 80, wanadai ya kuwa serikali ya kikoloni ya Uingereza iliwatesa na kuwapiga na baadhi ya jamaa zao walipoteza maisha kutokana na mateso hayo.
Kesi hiyo inatarajiwa kuanza mapema mwaka 2012.

No comments: